JUMLA ya shilingi bilinoni 5.4 zinatarajiwa kutumika katika ukarabati na utengenezaji wa barabara za Mkoa wa Tabora ambazo ziko chini ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA)
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt.Philemon Sengati wakati wa sherehe fupi ya kusaini mikataba ya ujenzi na ukarabati wa barabara kwa Wakandarasi na TARURA.
Alisema kiasi hicho ni awamu ya kwanza ya kiasi cha shilingi bilioni 7.1 iliyoidhinishiwa TARURA kwa mwaka wa fedha wa 2020/21 kwa ajili ya matengenezo ya barabara.
Dkt. Sengati alisema kazi zitakazofanyika ni pamoja na ujenzi wa kilimote 2.76 kwa kiwango cha lami , ujenzi wa makaravati zaidi ya mistari 59 na uchongaji wa barabara zaidi ya kilometa 541.
Aliwasihi Wakandarasi 34 walioshinda zabuni ya kutengeneza na kukarabati barabara hizo kufanyakazi kwa kuzingatia Sheria , kanuni na miongozo , ubunifu na weledi ili Serikali iendelee kuwa na imani nao na kuwapa kazi zaidi.
“Wakandarasi walioomba kazi ni wengi lakini nyie 34 tu ndio mmefanikiwa kupata nafasi …kwa hiyo msituangashe …tangulizeni mbele uzalendo kwa maslahi mapana ya Mkoa wa Tabora na Taifa kwa ujumla” alisisitiza.
Aliwataka Wakandarasi walioshinda kazi hiyo kuhakikisha kazi inakamilika ndani ya muda uliopangwa na kwa kuzingatia thamani halisi ya fedha iliyotolewa na Serikali.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora alimwagiza Mratibu wa TARURA na Wataalamu wake kuhakikisha wanasimamia kwa karibu miradi yote iliyopangwa ili ikamilike kwa viwango vilivypangwa.
Alisema Serikali inatoa fedha nyingi kwa miradi ya barabara , hivyo hatasita kumchukulia hatua Mtumishi ambaye atasababisha miradi kutekelezwa chini ya kiwango kwa kushindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo.
Dkt. Sengati alisema ujenzi wa miundombinu hiyo na mingine itachochea maendeleo katika sekta za utalii, kilimo.mifugo, uvuvi , viwanda na biashara.
Alisema hatua hiyo itasaidia kuimarisha kipato cha wakazi na Mkoa kwa ujumla na kufikia maono ya miaka mitano ijayo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ya kukuza uchumi kwa wasatani wa asilimia 8 .
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa