SERIKALI imezitaka Halmashauri zilizopo mkoani Tabora kupima maeneo na kuweka miundombinu itakayowawezesha kuyakodisha kwa wafugaji kwa gharama ya shilingi 3,500/- kwa ekari moja kwa mwaka kwa ajili ya malisho ya mifugo yao.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki wakati wa uzinduzi wa Kitabu cha Mwongozo wa uwekezaji cha Mkoa wa Tabora.
Alisema maeneo hayo yanatakiwa kuwa miundombinu ya majosho , malambo na huduma nyingine zinazotaji katika mifugo.
Waziri huyo wa Mifugo na Uvuvi alisema hatua itasaidia Halmashauri kuongeza mapato yao ya ndani badala ya kukimbizana na mama lishe na Machinga.
Ndaki alisema Mkoa wa Tabora unazo ng’ombe nyingi na Halmashauri zake zina maeneo makubwa ambapo yapingiliwa vizuri yatawasaidia kuepusha migogoro baina ya wafugaji na wakulima.
Aliongeza kuwa maeneo hayo yanaweza kutumika katika uboreshaji wa mifugo kwa ajili ya kuongeza tija ya uzalishaji wa nyama na maziwa.
Ndaki alisema ili Mwekezaji aweze kuweka Kiwanda cha Mazao ya mifugo ni lazima ajiridhishe upatikanaji wa bidhaa ya kutosha mwaka mzima.
Alisema suala la uboreshaji wa mifugo ni jambo la msingi kwa ajili ya kuwavutia wawekezaji katika sekta hiyo
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa