JUMLA ya wagonjwa 330 wa nje wamepata huduma ya matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Uyui tangu ilipoanza kutoa huduma hizo mwanzoani mwa mwezi huu.
Mganga Mkuu wa Wilaya(DMO) ya Uyui Dkt.Wilfred Rwechungura alisema idadi inahusu matibabu ya magonjwa mbalimbali ya wagojwa wa nje.
Dkt. Rwechungura alisema kwa wale wanahitaji matibabu zaidi ndio wanapa rufaa kwenda kupata huduma zaidi katika Hospitali nyingine.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora (Uyui) Hemed Magaro alisema walianza kutoa huduma hizo tangu walipoagizwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Sereikali za Mitaa.
Alisema ili kuanza utoaji huduma walihamisha baadhi ya Madaktari na Wauguzi kutoka maeneo mengine ili waweze kutoa huduma za matatibu katika Hopsitali hiyo ya Wilaya.
Mkazi wa Ilalasimba wilayani humo Lucia Kulwa aliishukuru Serikali kwa kuwasogezea huduma karibu yao.
Alisema hatua hiyo imewasaidia kuondokana na adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu katika Hopsiali ya Ndala iliyopo wilayani Nzega na wengine walisafiri hadi Manispaa ya Tabora kwenda kutibiwa katika Hospitali ya St. Anne iliyopo Ipuli na wengeni katika Hospitali ya Rufaa Kitete.
Naye Mkazi wa Isikizya Halima Swed alisema wanapata huduma nzuri kutoka kwa madkatari na wauguzi tangu ilipofunguliwa tarehe 8 Mwezi huu.
Aliiomba Serikali kuisaidia vifaa ili huduma za wagonjwa wa kulazwa na upusuaji ziweze kufanyika Hopsitalini hapo badala ya kwenda Kitete na Ndala ili kupata huduma hizo.
“Tunaishukuru sana Serikali ya Rais Magufuli kwa kutuona wakazi wa Uyui na kutujengea Hospitali ya Wilaya …tunawaomba watuletee vitanda vya wagonjwa na vifaa vingine ili kama mtu anatakiwa kulazwa alazwe hapa hapa badala ya kwenda Upuge au Ndala ili kupunguza gharama za wanaomhudumia mgonjwa” alisema.
Hospitali ya Wilaya ya Uyui ina jumla ya Madkatari watano na Wauguzi watatu ambao ndio wanasaidia utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa nje.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa