WAKAZI wa Manispaa ya Tabora wameiomba Serikali kuajiri watumishi wapya wa kada mbalimbali katika sekta ya afya ili kuboresha utoaji wa huduma katika Zahanati zilizopo katika maeneo mengi.
Wakazi hao wametoa ombi hilo jana kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora aggrey Mwanri wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa shughuli za Malipo kwa Ufanisi (RBF) kwenye Vituo na Zahanati mbali katika Manispaa hiyo.
Mkazi wa Kidongo Chekundu Kata ya Ng’ambo Fatuma Kazomba alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa pamoja na kuwa wanapata Wauuguzi wanawahudumia vizuri lakini wamekuwa wakitumia muda mwingi kupata huduma katika Zahanati yao ya Ng’ambo kutokana na uchache wa watumishi.
Alisema hali hiyo imefanya baadhi yao kuzidiwa wakiwa wanasubiri huduma na wengine kukimbilia katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete.
Naye Leah Francis wa Kalunde alisema kuwa katika Zahanati yao wanae mtumishi mmoja ambaye ni Mganga Mfawidhi jambo linalofanya huduma kwenda polepole pindi kunapokuwepo na wagonjwa wengi.
Aliomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuajiri watumishi wapya ili kuziba pengo lilipo.
Akijibu hoja hizo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri aliiagiza uongozi wa Manispaa ya Tabora kuangalia sehemu ambayo ina watumishi wengi na kupeleka kwenye upungufu mkubwa wakati Serikali ikiendelea kuajiri.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa