Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian awasilisha taaarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 Halmashauri kuu ya CCM(M) Tabora.
Pamoja na mambo mengine Mh. Mkuu wa Mkoa,alieleza kuwa kwa kipindi cha miaka miwili ya Mh. Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mkoa wa Tabora umeendelea kutekeleza ilani ya CCM kwa mafanikio makubwa sana katika sekta ya elimu, afya, kilimo miundombinu ,maji, bandari kavu na reli ya kisasa.
Mh Mkuu wa Mkoa, akifafanua ,alisema, katika sekta ya Elimu mkoa umepokea shilingi Bilioni 41.1 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya, madarasa sambamba na uboreshwaji wa mazingira ya shule. Lakini pia uanzishwaji wa vyuo vya ufundi wilaya ya Uyui na Nzega . Na hivyo mkoa umefanikiwa kutoa nafasi ya watoto na vijana kupata elimu na ujuzi.
Na katika sekta ya Afya mkoa ulipata shilingi Bilioni 21.06, kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za wilaya ,vituo vya afya . Zahanati pamoja na ununuzi na ukarabati wa vifaa tiba. Uboreshwaji huo umewezesha mkoa kutoa huduma ya afya kwa uhakika na kupunguza vifo vya wamama wajawazito na watoto.
Kwa sekta ya maji mkoa ulipokea Bilioni 640 kwa ajili ya kutoa maji ziwa victoria hadi Tabora na kuufanya mkoa kufikia asilimia 62.4 huduma ya maji vijijini na asilimia 75.3 kwa mijini.
Aidha kwenye Kilimo Mkoa ulipata shilingi Bilioni 24.79 zilizotumika kwenye miradi mbalimbali ya kilimo ikiwemo ujenzi wa mifumo ya kisasa ya umwagiliaji na utoaji wa ruzuku kwenye mbolea.
Upande wa barabara mkoa ulipokea shilingi Bilioni 359 ambazo zilitumika kujenga mtandao wa barabara wenye urefu wa Km 266.71. Sambamba na hilo uboreshwaji wa barabara vijijini na mijini.
Mkoa ulipokea Trilioni 4.406 kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Makutupora-Tabora wenye urefu wa Km 368.
Aidha, Mkoa umefanikiwa kwenye sekta ya Umeme utunzaji wa mazingira , Mawasiliano, bandari kavu na uwezeshwaji wananchi kiuchumi. Alisema Mafanikio haya yanalenga kubadilisha maisha ya mwananchi mmoja mmoja wa Mkoa wa Tabora. Na ndiyo dhamira ya Serikali ya awamu ya sita.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa