• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

DKT. JOHN MBOYA AKAGUA MAENEO YALIYOATHIRIWA NA MAFURIKO TABORA, ATOA WITO WA TAHADHARI NA UZINGATIAJI WA SHERIA ZA UJENZI

Posted on: December 22nd, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, amefanya ziara ya kukagua hali ya maeneo ya kata za Mwinyi na Malolo yaliyoathiriwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua za masika zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini.

                   

Akizungumza na wananchi pamoja na viongozi wa kata ya Malolo, Dkt. Mboya amepongeza uongozi wa Manispaa ya Tabora ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji pamoja na Mstahiki Meya kwa kuchukua hatua za haraka kushughulikia athari za mafuriko hayo, hatua zilizosaidia kunusuru makazi ya wananchi na kuimarisha usalama wao.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kubwa katika kulinda usalama wa maisha na mali zao, hususan katika kipindi hiki ambacho mvua za masika zinaendelea kunyesha nchini. Vilevile, amewakumbusha viongozi wa mamlaka za serikali za mitaa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria, taratibu na kanuni za ujenzi, akisisitiza umuhimu wa kuepuka utoaji wa vibali vya ujenzi katika maeneo hatarishi yanayotuamisha maji.

Akieleza chanzo cha mafuriko, Kaimu Meneja wa TARURA Mkoa wa Tabora, Mhandisi Subira Manyama, amesema mvua kubwa ilisababisha maji kukosa njia za kupita kutokana na barabara kuwa bado katika hatua za ukamilishaji na hivyo kuingia kwenye makazi ya wananchi. Ameeleza kuwa TARURA tayari imeanza kukamilisha mitaro na kujenga njia za muda mfupi, huku kazi hiyo ikitarajiwa kukamilika ndani ya siku mbili.

Kwa upande wao, viongozi wa kata hizo pamoja na wananchi wameishukuru Serikali kwa hatua za haraka zilizochukuliwa kukabiliana na athari za mafuriko, wakieleza kuwa jitihada hizo zimeongeza imani ya wananchi na kuimarisha ushirikiano kati ya jamii na serikali katika nyakati za dharura.

Katika hatua nyingine, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tabora, Afande Laizer, amesema jeshi hilo lipo tayari kutoa huduma za uokozi muda wote. Amewahimiza wananchi kutoa taarifa mapema pindi yanapotokea maafa yanayotokana na mvua, kwa kutumia namba ya dharura ya bure 114, ili hatua stahiki zichukuliwe kwa wakati.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DKT. JOHN MBOYA AKAGUA MAENEO YALIYOATHIRIWA NA MAFURIKO TABORA, ATOA WITO WA TAHADHARI NA UZINGATIAJI WA SHERIA ZA UJENZI

    December 22, 2025
  • MHE. PAULO CHACHA APOKEA UWEKEZAJI MKUBWA WA UJENZI WA KIWANDA CHA MBOLEA UTAKAONUFAISHA WAKULIMA WA NDANI NA NJE YA MKOA WA TABORA

    December 05, 2025
  • MHE. CHACHA AFUNGUA MKUTANO WA TAPSHA MKOA, ATOA WITO KWA WALIMU KUJIENDELEZA KIELIMU ILI KUWA MAHILI KATIKA UTENDAJI KAZI WAO.

    December 02, 2025
  • MHE. CHACHA ACHUKUA HATUA ZA KISHERIA BAADA YA KUBAINI UBADHILIFU KATIKA MRADI WA UJENZI WA SOKO KUU TABORA

    December 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa