• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KABLA YA NDOA WANANCHI TUJENGE UTARATIBU WA KUPIMA SELIMUNDU ILI KUZUIA MNYORORO WA UGONJWA HUU NCHINI – DKT. MBOYA

Posted on: March 7th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, ameongoza uzinduzi wa mradi wa kupambana na ugonjwa wa selimundu (Sickle Care) katika ukumbi wa mikutano wa Isike, Mwanakiyungi. Zoezi hili linatokea katika wakati muhimu ambapo mkoa wa Tabora umeendelea kuwa na kiwango kikubwa cha wagonjwa wa ugonjwa huu.

Akitoa taarifa kuhusu hali ya ugonjwa wa selimundu mkoani Tabora, Katibu Tawala Msaidizi wa Afya, Dkt. Honoratha Rutanisibwa, alieleza kuwa selimundu ni ugonjwa wa kurithi unaoathiri seli nyekundu za damu. Alisema kuwa mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa nchini yenye kiwango kikubwa cha wagonjwa, ambapo mwaka 2023 mkoa huu ulikuwa na wagonjwa 6,384, na mwaka 2024 idadi ya wagonjwa iliongezeka hadi kufikia 8,465.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Melian Foundation, Bw. Samwel Mabewa, aliishukuru serikali kwa ushirikiano mkubwa kutoka kwa Wizara ya Afya, TAMISEMI, pamoja na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa  ushirikiano walioupata  na kuwa umeongeza ufanisi katika kupambana na ugonjwa wa selimundu.

Mradi wa Sickle Care, una lengo la kutoa elimu sahihi kuhusu ugonjwa wa selimundu, ili wananchi waweze kuelewa na kutouhusianisha na imani za kishirikina. Aidha, mradi huu utawezesha upimaji na utambuzi wa mapema wa ugonjwa wa selimundu kwa watoto chini ya miaka mitano, jambo litakalosaidia kutibu ugonjwa huu kwa urahisi. Vilevile, mradi huu utatoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ili waweze kumudu vizuri katika kukabiliana na ugonjwa wa selimundu katika maeneo yao.

Afisa kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Bw. Kalidushi Charles, alitoa rai kwa mamlaka za serikali za mitaa kuongeza juhudi katika kupambana na ugonjwa huu kwa kutenga bajeti ya kusaidia juhudi za serikali na wadau katika kupambana na ugonjwa wa selimundu.

Dkt. Hamad Nyembea, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka Wizara ya Afya, alieleza kuwa wizara hiyo ina mikakati madhubuti ya kinga na tiba dhidi ya ugonjwa wa selimundu, ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa umma, kuwahamasisha wananchi kupima na kujua hali zao, na kuanza matibabu mapema, hasa kutokana na ongezeko kubwa la ugonjwa huu kwa miaka ya hivi karibuni.

Akizungumza katika uzinduzi wa huduma hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, alisisitiza umuhimu wa waganga wakuu wa halmashauri kusimamia mradi huu kwa umakini, ili utekelezwe kwa ufanisi mkubwa na kuleta matokeo chanya katika kupunguza athari za ugonjwa wa selimundu. Aliongeza kuwa ni muhimu kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ugonjwa huu na hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kudhibiti ugonjwa wa selimundu.

Dkt. Mboya alihitimisha zoezi la uzinduzi kwa kugawa vifaa kwa wataalam wa afya, ikiwa ni pamoja na dawa na mashine za kuthibitisha uwepo wa ugonjwa huo. Mradi huu wa Sickle Care unadhaminiwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la Melian Foundation kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Afya. Zoezi hili la uzinduzi linatarajiwa kuwa na manufaa makubwa kwa jamii ya mkoa wa Tabora na kusaidia katika juhudi za kupambana na ugonjwa wa selimundu nchini.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa