Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani amewataka wakazi wa wilaya ya Kaliua kutunza mazingira hasa yale maeneo yenye vyanzo vya maji.
Akiongea na wananchi wa kata ya Mwongozo, Dkt. Batilda ameiomba TFS (W) Kaliua Kusimamia zoezi la upandaji miti sambamba na utolewaji wa elimu ya mazingira kwa wananchi.
Aidha, Dkt. Batilda amewataka watendaji wa Kata na vitongoji kusoma taarifa za miradi ya maendeleo kwa wananchi wao ili wananchi hao wafahamu kazi zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Asisitiza wananchi wa kata hiyo na Tabora kwa ujumla juu ya suala la kuwaandikisha watoto wanaopaswa kujiunga na kidato cha kwanza Mwaka huu.
Awataka vijana kutambua fursa zilizopo mkoani Tabora, awashauri kuanzisha viwanda vidogovidogo kwa kutumia Malighafi kutoka Tabora ambavyo vitaleta faida kwa jamii.
Akiambatana na kamati ya Ulinzi na Usalama (M) Tabora, nao walikuwa na haya ya kusema:
Mkurugenzi wa TAKUKURU (M) Tabora Ndugu. Musa Chaula awataka wananchi wa Tabora kuelewa kuwa majukumu ya chombo hicho sio tu kukamata bali pia linajukumu la kutoa elimu kwa Umma.
Awataka watumishi wa Umma mkoani Tabora kutumia vema fedha zinazotolewa na Serikali katika miradi mbalimbali ya maendeleo. Na pia alisisitiza mikakati mipya ya TAKUKURU katika kukabiliana na vitendo vya rushwa mkoani Tabora.
naye kaimu Kamishina wa Uhamiaji (M) Tabora Ndugu. Agustino Malembo amewataka wananchi wa Tabora kutoa taarifa za ndugu na jamaa ambao wanafika kwenye maeneo yao kwa lengo la kuepuka vitendo vya uhalifu pamoja na magonjwa ya kuambukizwa yanayoweza kuletwa na wahamiaji haramu hao.
Pia, Kaimu Mshauri wa Jeshi la Akiba (M) Tabora Mej. Method Nkangaza, amewashauri vijana kujiunga na mafunzo ya jeshi la Akiba ambalo limekuwa namafunzo mengi ambayo yamekuwa na mchango mkubwa katika kukuza uchumi. Na kwamba mafunzo hayo yamekuwa na msaada mkubwa sana kwa vijana katika kubuni na kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo hasa shughuli za ujasiriamali.
Naye Kamanda wa Polisi (M) Tabora RPC Richard Abwao, amewataka wenyeviti wa vijiji na vitongoji kushirikiana katika masuala ya Ulinzi na Usalama.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa