• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MHE. CHACHA AFUNGUA MKUTANO WA TAPSHA MKOA, ATOA WITO KWA WALIMU KUJIENDELEZA KIELIMU ILI KUWA MAHILI KATIKA UTENDAJI KAZI WAO.

Posted on: December 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, amefungua rasmi Mkutano Mkuu wa siku mbili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara (TAPSHA) ngazi ya mkoa, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondaro Themi Hill, mjini Tabora. Mkutano huo umebeba umuhimu mkubwa katika kuboresha uongozi wa elimu na kuimarisha ushirikiano miongoni mwa walimu wakuu.

Akizungumza wakati wa utangulizi, Mwenyekiti wa TAPSHA Mkoa wa Tabora, Iddy Gunto, alisema umoja huo umeanzishwa ili kuwaunganisha walimu wakuu wote wa shule za msingi nchini. Alibainisha kuwa kupitia TAPSHA, mkoa umeimarisha usimamizi wa taaluma na kuongeza ufaulu, hali iliyofanya Tabora kushika nafasi ya 16 kitaifa kwa asilimia 81.1. Aliongeza kuwa wanamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kulindaa maslahi ya walimu, ikiwa ni pamoja na upandishaji vyeo na stahiki zingine.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Mkoa wa Tabora, Mwl. Upendo Rweyemamu, alisema mkutano huo unalenga kufanya tathmini ya  utekelezaji shughuli za taaluma shuleni kwa mwaka 2025 na kuweka mikakati ya pamoja ili kuboresha ufaulu kwa mwaka wa masomo 2026. Aidha alisisitiza kuwa mkutano huo utawajengea uwezo walimu wakuu katika maeneo ya udhibiti ubora pamoja na masuala yanayohusiana na Tume ya Utumishi wa Walimu.

Kwa upande wake,Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, amewapongeza walimu na wazazi kwa ushirikiano uliowezesha mkoa kupata matokeo mazuri kitaifa. Aliwataka walimu wakuu kuimarisha mahusiano na wazazi, kuhakikisha upatikanaji wa chakula shuleni, na kujenga mawasiliano yenye staha baina ya walimu na viongozi wao, akisisitiza kuwa motisha na mazingira bora ya kufundishia ni nguzo muhimu za ufaulu.

Akiwahutubia maelfu ya walimu wakuu pamoja na viongozi wa elimu ngazi ya mkoa na wilaya, Mgeni Rasmi Mhe. Chacha aliwahimiza walimu wakuu kuendeleza umoja wao kwa weledi. Alikabidhi mchango wa shilingi milioni 10 kwa TAPSHA ili kuimarisha mfuko wa umoja huo, huku akiwahimiza watumishi kujiendeleza kielimu. Alisisitiza kuwa umahiri katika utendaji hutokana na kuongeza ujuzi, kusoma na kufanya utafiti wa mara kwa mara, sambamba na kujituma katika majukumu ya kila siku.

Mkutano huo ulihusisha walimu wakuu wote wa shule za msingi mkoa wa Tabora pamoja na maafisa elimu kata, ukiwa chini ya kaulimbiu “Matokeo Bora 2026, Inawezekana – Timiza Wajibu Wako.” Kaulimbiu hiyo inalenga kuongeza ufanisi wa sekta ya elimu na kuhimiza uwajibikaji katika ngazi zote.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AFUNGUA MKUTANO WA TAPSHA MKOA, ATOA WITO KWA WALIMU KUJIENDELEZA KIELIMU ILI KUWA MAHILI KATIKA UTENDAJI KAZI WAO.

    December 02, 2025
  • MHE. CHACHA ACHUKUA HATUA ZA KISHERIA BAADA YA KUBAINI UBADHILIFU KATIKA MRADI WA UJENZI WA SOKO KUU TABORA

    December 01, 2025
  • MAHAFALI YA 11 AMUCTA: DKT. MBOYA AWAASA WAHITIMU KUITUMIA ELIMU WALIYOIPATA KWA MAENDELEO YA TAIFA

    November 29, 2025
  • “WATAALAMU WA KILIMO TWENDENI TUKASIMAMIE UZALISHAJI KWA KUZINGATIA UTABIRI WA HALI YA HEWA.” DKT. MBOYA

    November 06, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa