• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MHE. CHACHA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI WILAYANI URAMBO: KWA KUFANYA USAFI, KUPANDA MITI NA KUTOA WITO WA KUTUNZA MAZINGIRA.

Posted on: June 5th, 2025

MHE. CHACHA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI WILAYANI URAMBO: KWA KUFANYA USAFI, KUPANDA MITI NA KUTOA WITO WA KUTUNZA MAZINGIRA.

Na. Robert Magaka – Urambo, Tabora.

Katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, ameongoza mamia ya wananchi wa Mkoa wa Tabora kushiriki katika shughuli za usafi na upandaji miti katika stendi kuu ya mabasi ya wilaya ya Urambo, ikiwa ni sehemu ya kuhimiza ulinzi na uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaliua, Ndugu Raymond Mweli, aliwapongeza watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora pamoja na watendaji wa wilaya zote kwa kuendeleza utekelezaji wa sera ya taifa ya uhifadhi wa  mazingira.

“Hakuna maendeleo,hakuna maisha bora bila kuwa na afya bora, ni wajibu wetu sisi sote,kuendelea kuhifadhi mazingira yetu,kuhakikisha tunaelimishana juu ya umuhimu wa kuendelea kuhifadhi mazingira yetu.”  alisema Mweli.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Urambo, Mhe. Margareth Sitta, aliwashukuru  wananchi kwa ushirikiano wao. Pia aliiomba serikali kupitia TANROADS kuunganisha kwa kiwango cha lami kipande cha barabara kinachotoka stendi hadi barabara kuu ya Kaliua ili kuwezesha mabasi kufika stendi kwa urahisi zaidi na kuongeza mapato ya halmashauri.

Akihutubia hadhira hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Paul Chacha aliwataka wananchi kuendelea kushiriki katika jitihada za kuhifadhi mazingira huku akisisitiza kuwa mazingira safi na salama ni msingi wa maendeleo endelevu.

"Napenda mtambue kwamba matumizi ya kuni na mkaa hapa nchini Tanzania yanaathiri sana hali ya misitu yetu.,Hali hii inachangia uharibifu wa ardhi pamoja na vyanzo vya maji hivyo tunapaswa kutumia nishati safi ya kupikia ili kupunguza athari katika misitu na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi" alisisitiza Mhe. Chacha.

Katika hatua nyingine, Mhe. Chacha aliipongeza Wilaya ya Sikonge kwa kupiga hatua kubwa katika maandalizi ya biashara ya hewa ya ukaa, akibainisha kuwa kila wilaya ya mkoa wa Tabora inapaswa kuwa na mpango huo ili kuchangia uchumi wa taifa na kuhifadhi mazingira.

Aidha, aliiagiza TANROADS kushughulikia suala la barabara ya kuingia stendi ya Urambo kama jambo hilo lilivyoelezwa na Mhe. Sitta, pamoja na halmashauri kuangalia upya viwango vya upangishaji wa vibanda vya biashara ili viwe rafiki kwa wananchi wa kipato cha chini.

Katika kumaliza hotuba yake, Mhe. Chacha alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi thabiti unaoendelea kuwaletea maendeleo Watanzania, akisema wananchi wa Tabora ni mashahidi wa mageuzi makubwa yanayofanyika nchini.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC CHACHA AONGOZA OPARESHENI YA KUTEKETEZA SHAMBA LA BANGI KATIKA ENEO LA HIFADHI YA NYAHUA MBUGA SIKONGE.

    June 06, 2025
  • MHE. CHACHA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI WILAYANI URAMBO: KWA KUFANYA USAFI, KUPANDA MITI NA KUTOA WITO WA KUTUNZA MAZINGIRA.

    June 05, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI - JUNI 5, 2025.

    June 04, 2025
  • SERIKALI YATOA SHILINGI BILIONI 26.9 KUWAINUA WAKULIMA KUPITIA MRADI WA UMWAGILIAJI MWAMAPULI – IGUNGA

    June 03, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa