Leo Tarehe Septemba 14, 2023 Ndugu Abdallah Shaibu Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, amezindua mradi wa usambazaji maji wenye thamani ya shilingi zaidi ya milioni mia nne zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maji uliopo Sikonge ambao unanufaisha wakazi wa kata ya Sikonge na Misheni.
Ndugu Abdallah Shaibu Kim Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru amesema ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huu kwakuwa umefuata taratibu zote muhimu ikiwepo kufanya tathmini ya athari za kimazingira katika eneo la mradi na nyaraka zote za mradi zipo.
Aidha amewaeleza wananchi kuwa Serikali ina dhamira ya dhati kabisa kuhakikisha wananchi wote wanapata maji safi na salama.
Mwisho kabisa mradi huu umezinduliwa rasmi na Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru 2023 ndugu Abdallah Shaibu Kim na kufurahi zaidi kwakuwa mradi huu uliwekewa jiwe la msingi mwaka Jana 2022 na Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa