• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

Posted on: July 1st, 2025

Na. Robert Magaka – Tabora.

 

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Matiko Chacha, ameongoza hafla ya kuwaapisha wakuu wa wilaya wapya pamoja na viongozi wengine waandamizi, akiwataka kuzingatia maadili, weledi, na uadilifu katika utumishi wao kwa umma.

Katika tukio hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtemi Isike Mwanakiyungi, walioapishwa  rasmi ni Mhe. Upendo Bert Wella aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora na Mhe. Thomas Mendraid Myinga, Mkuu mpya wa Wilaya ya Sikonge. Viongozi hao waliapishwa sambamba na wakurugenzi na makatibu tawala wapya wa wilaya, ambapo wote walikula kiapo cha uadilifu katika utumishi wa umma.

Viongozi wengine waliokula kiapo cha uadilifu mbele ya Mkuu wa Mkoa ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, Ndg. Mwarami Seif, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua, Ndg. Shaban Kabelwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Tabora, Dkt. Marco Pima, pamoja na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaliua, Ndg. Sosthenes Chakupanyuka.

Akizungumza kwa niaba ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Ndg. Said Juma Nkumba, aliwataka viongozi hao kufuata kwa karibu maelekezo ya serikali, kuwa na ushirikiano na watumishi waliowakuta, na kumtanguliza Mungu katika majukumu yao ya kila siku.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, aliwataka viongozi hao kutambua kuwa uteuzi wao ni heshima na imani kubwa waliyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Mboya aliwataka kwenda kusimamia miradi ya maendeleo, kudhibiti matumizi ya fedha za umma kwa mujibu wa sheria za fedha na manunuzi ya umma, pamoja na kushughulikia miradi viporo. Alisisitiza umuhimu wa kusimamia mazingira na mapato ya halmashauri kwa uwazi na

Akihitimisha hafla hiyo,Mhe. Chacha aliwataka viongozi hao kutanguliza bidii na uadilifu katika kazi zao, hasa ikizingatiwa kuwa taifa linaelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu. Amesisitiza viongozi hao kuepuka kusimama katika upande wowote ule ambapo wagombea watafika katika maeneo yao kwa nia ya kutangaza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Viongozi hao pia waliagizwa kuendeleza mambo mazuri yaliyoanzishwa na watangulizi wao na kuwa mstari wa mbele kulinda na kuimarisha amani, mshikamano, na maendeleo ya wananchi.

Kwa upande wao viongozi hao wameahidi kwenda kufanya kazi kwa bidii na kuwatumikia wananchi na kwamba watakwenda kuwa wasaidizi wazuri katika uongozi wa mkoa wa Tabora.

“Nakuadi tuliopishwa leo na wengine walioko hapa wote hatutakuangusha,tutafanya kazi kuwatumikia wananchi maana lengo kuu la serikali nikuleta ustawi kwa wananchi, tutakuwa wasidizi wazuri kwako wakati wote.” Alieleza Mhe. Myinga.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa