• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

Posted on: May 1st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Mheshimiwa Sauda Mtondoo, amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mheshimiwa Paul Chacha, katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani,Mei  1, 2025,yaliyofanyika kimkoa  Uwanja wa Samora katika Halmashauri ya Mji wa Nzega.

Akisoma risala kwa niaba ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Mkoa wa Tabora (TUCTA), Mwalimu Silas John Mbuluma alieleza kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kuwaleta pamoja wafanyakazi na waajiri ili kutathmini mafanikio ya mwaka uliopita, kujadili changamoto zilizopo, na kuweka mikakati ya kuboresha mazingira mahala pa kazi. Pia, alisema ni fursa ya kuhimiza nidhamu kazini na kuwakumbusha kuhusu sheria ya ajira na mahusiano kazini.

Mwalimu Mbuluma amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ajira mpya katika sekta mbalimbali, hatua iliyowezesha kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi. Hata hivyo, walieleza changamoto zinazoikabili sekta ya umma, hasa katika kada ya elimu na afya, zikiwemo miundo ya utumishi isiyowahamasisha watumishi kujiendeleza kielimu, mishahara midogo isiyokidhi gharama za maisha, na kiwango kikubwa cha kodi (PAYE) kwenye mishahara yao.

Wafanyakazi pia waliitaka Serikali kufanyia kazi suala la leseni za kitaaluma zinazolipiwa kila mwaka na watumishi wa afya, wakipendekeza mzigo huo ubebwe na mwajiri. Aidha, walilalamikia utaratibu duni wa utoaji wa mikataba ya ajira, kunyimwa ruhusa, kutothibitishwa kazini, malimbikizo ya madeni, mapunjo ya mishahara, na huduma hafifu za bima ya afya licha ya makato kuendelea kufanyika kwa kiwango kilekile.

Akihutubia maelfu ya wafanyakazi na wananchi wa Nzega, Mheshimiwa Mtondoo alisema Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa wafanyakazi katika maendeleo ya taifa. "Haki na maslahi ya wafanyakazi ni jambo lisilopaswa kupuuzwa. Wafanyakazi ni uti wa mgongo wa taifa letu. Bila wao, hakuna maendeleo," alisisitiza.

Mheshimiwa Mtondoo aliwataka wafanyakazi kutumia busara kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa kuchagua viongozi waadilifu, wachapakazi na wanaojali maslahi ya wafanyakazi. Alihimiza ushiriki wa wafanyakazi katika mchakato wa uchaguzi kwa kujiandikisha na kuhakiki taarifa zao ili waweze kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi sahihi. Pia aliwakumbusha kuwa, kwa mujibu wa sheria, wafanyakazi wana haki ya kugombea nafasi za uongozi.

Kuhusu suala la mishahara na marupurupu, Mheshimiwa Mtondoo alieleza kuwa Serikali inaendelea kujipanga ili kuboresha viwango vya mishahara na kuendeleza majadiliano na waajiri kupitia vyama vya wafanyakazi. Aidha, alisisitiza kuwa Serikali inapinga vikali aina yoyote ya unyonyaji na unyanyasaji kazini, na inaendelea kuwekeza katika mafunzo na ujuzi kwa wafanyakazi ili kuongeza tija katika utumishi wa umma.

Mhe. Mtondoo amemuelekeza Katibu Tawala wa mkoa kushughulikia kwa haraka changamoto zinazowezekana kutatuliwa katika ngazi ya mkoa, huku zile zilizo nje ya uwezo wake zikipelekwa kwenye mamlaka husika.

Akihitimisha hotuba yake, Mheshimiwa Mtondoo alitoa wito kwa wafanyakazi wote nchini kuzingatia haki na wajibu wao kwa uadilifu na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao ya  kila siku.

 Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni: "Uchaguzi Mkuu 2025, Utuletee Viongozi Wanaojali Haki na Maslahi ya Wafanyakazi – Sote Tushiriki."

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WIZARA YA AFYA NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA TABORA YAENDESHA KIKAO ELEKEZI CHA MREJESHO WA MAFUNZO NA MAPITIO YA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

    May 14, 2025
  • JESHI LA POLISI TABORA LAPATA MAGARI 6 MAPYA KWA AJILI YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

    May 12, 2025
  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa