• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

Posted on: June 26th, 2025

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Ndg.Asanterabi Sang’enoi, ameongoza Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtemi Isike Mwanakiyungi.

Katika ufunguzi wa mkutano huo, Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Bi. Monica Yesaya, aliwapongeza wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) kwa mchango wao mkubwa katika kusukuma gurudumu la maendeleo. Alisisitiza umuhimu wa mashirika hayo kuwasilisha kwa wakati taarifa za utekelezaji wa shughuli zao kila robo mwaka ili kuwezesha kufanyika kwa tathmini ya mchango wao katika jamii.

Kwa upande wake, Bi. Agneta John kutoka Shirika la JIDA, akizungumza kwa niaba ya NGO’s mkoa wa Tabora, alieleza changamoto zinazoathiri ufanisi wa mashirika hayo, zikiwemo gharama kubwa za uendeshaji, ukosefu wa fedha na rasilimali watu, pamoja na baadhi ya watumishi wa ofisi za umma kushindwa kutoa ushirikiano kwa mashirika hayo. Alitoa ombi kwa serikali kuweka mazingira wezeshi ya upangishaji wa majengo ya serikali kwa bei nafuu, sambamba na kutoa maelekezo kwa watumishi wa umma kutoa ushirikiano kwa wadau wote wa maendeleo wanaofika katika ofisi za umma kupata huduma mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ndugu Asanterabi Sang’enoi alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuimarisha mazingira wezeshi kwa mashirika yote yanayotoa huduma kwa wananchi. Alisisitiza umuhimu wa uwazi, uwajibikaji na ushirikiano baina ya mashirika na serikali, hasa katika kutekeleza shughuli za kijamii kama vile uchangiaji damu, usafi wa mazingira, upandaji miti, na kusaidia makundi maalum kama wagonjwa na watoto yatima.

“Sheria hairuhusu mashirika yasiyo ya kiserikali kujihusisha na siasa. Kwa yale yatakayopata vibali vya kutoa elimu ya mpiga kura, yahakikishe yanazingatia sheria, taratibu, kanuni na miongozo ya Tume Huru ya Uchaguzi,” alisema Sang’enoi. Alisisitiza kuwa kila Mtanzania ana wajibu wa kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, huku akihimiza kulinda amani kama tunu ya taifa.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Afisa Uchunguzi kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Mkoa wa Tabora, Ndg. Patrick Shayo, ambaye alitoa mada kuhusu nafasi ya mashirika yasiyo ya kiserikali katika kukuza maadili nchini. Aliyasihi mashirika hayo kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia mila, desturi, sheria na maadili ya Kitanzania. “Hatutarajii kuona mashirika yanayokiuka misingi ya utamaduni wa taifa letu, ikiwemo kuhamasisha ndoa za jinsia moja,” alionya.

Afisa Maendeleo wa Mkoa, Bw. Elias Mpangala, alihitimisha kwa kusisitiza kuwa mikutano kama hiyo ni ya kisheria na yenye tija, kwani huleta jukwaa la mashauriano baina ya serikali na NGO’s, hali inayowezesha kubaini mafanikio na changamoto kwa lengo la kuboresha huduma kwa wananchi.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • SERIKALI YAJIPANGA KUIMARISHA HUDUMA ZA UGONJWA WA SIKO SELI NCHINI.

    June 19, 2025
  • “TUSIRUHUSU KIWANGO CHA ADHABU KISICHO NA KIASI KWA MTOTO – MHE.TUKAI AONYA

    June 16, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa