• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TUITUNZE MIUNDOMBINU YA MAWASILIANO KWA MAENDELEO YETU – MHANDISI MAHUNDI.

Posted on: March 26th, 2025

Na Mwandishi Wetu – Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tabora.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amefanya ziara mkoani Tabora kukagua hali ya mawasiliano katika wilaya za Uyui na Tabora Manispaa. Ziara hiyo imelenga kujiridhisha na upatikanaji wa huduma za mawasiliano, pamoja na kuhimiza wananchi kutunza miundombinu ya mawasiliano kwa manufaa ya maendeleo yao.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya mawasiliano katika mkoa wa Tabora, Meneja wa TCRA Kanda ya Kati, Mhandisi Asajile John, alisema kuwa TCRA inaendelea kusimamia usambazaji wa huduma za mawasiliano kwa kuzingatia jiografia na idadi ya watu. Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 98 ya wananchi wa Tabora wanapata mawasiliano ya 2G, asilimia 81.6 wanapata 3G, asilimia 72.1 wanatumia 4G, huku asilimia 3.2 wakifikiwa na mtandao wa 5G. Aidha, kwa ujumla asilimia 91 ya Watanzania wanapata huduma za 3G, hatua inayowezesha wananchi  kuingia katika uchumi wa kidijiti. Kufikia Desemba 2024, Tabora ilikuwa na laini za simu milioni 4.28, idadi inayozidi wakazi wa mkoa huo kwa asilimia 123.8 kulingana na sensa ya mwaka 2022.

Katika hatua nyingine, vitendo vya uhalifu mtandaoni vimepungua kwa asilimia 79.3 mwaka 2024 ikilinganishwa na 2023, ambapo kulikuwa na rekodi ya majaribio 590 ya uhalifu mtandaoni. Mafanikio haya yanatokana na juhudi za serikali kutoa elimu kwa umma kuhusu usalama  mtandaoni.

Mhe. Mahundi alitembelea ujenzi wa minara ya mawasiliano inayojengwa kwa ushirikiano wa sekta binafsi na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF). Mnara wa mtandao wa Yas unaojengwa kwa gharama ya shilingi milioni 290 katika kata ya Ifucha, Manispaa ya Tabora, pamoja na mnara wa Halotel unaojengwa katika kijiji cha Mwakashindye, kata ya Ibiri, wilayani Uyui, ni miongoni mwa juhudi za kuimarisha mawasiliano nchini.

Katika hotuba yake, Mhe. Mahundi aliwataka wananchi kuitunza miundombinu hiyo na kuzingatia matumizi sahihi ya teknolojia kwa maendeleo yao, huku akiwatahadharisha wananchi kuepuka kuwa sehemu ya watu wanaoihujumu serikali kwa kuharibu miundombinu  hiyo.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Kanda ya Kati, Ndg. Shirikisho Mpunji, alisema kuwa serikali imeendelea kujenga minara ya mawasiliano katika maeneo yenye changamoto. Hadi sasa, minara 118 yenye thamani ya shilingi bilioni 19 imekamilika katika kata 86 za Tabora, huku awamu ya tisa ya ujenzi wa minara mingine ikitarajiwa kutangazwa hivi karibuni.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini, Mbunge wa jimbo hilo, Mhe. Almasi Maige, aliishukuru serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka zaidi ya shilingi bilioni 2.2 kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika sekta za afya, elimu na miundombinu, hatua inayowanufaisha wakazi wa wilaya ya Uyui kwa kiasi kikubwa.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa