Tabora Manispaa.
21/02/2023
__________________
Mkuu wa mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, amefungua kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa. Kikao ambacho kimehudhuriwa na viongozi wote wa ngazi ya mkoa na wilaya, viongozi wa CCM, viongozi wa dini na wadau wa maendeleao ya mkoa wa Tabora.
Akitoa hutuba yake Dkt. Batilda alianza kwa kumshukuru Rais wa Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi ambazo zimetumika kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa madarasa mapya, ujenzi wa hospitali za wilaya, zahanati, ujenzi wa reli wa kisasa yaani SGR, ruzuku kwenye pembejeo za kilimo, ujasiliamali, ujenzi wa bomba la mafuta, usambazwaji wa maji na miradi mingine mingi ambayo serikali ya awamu ya sita inaendelea kuitekeleza.
Aidha amewataka wajumbe wa kikao hiko kuweka mkazo suala la utunzaji wa mazingira. Kama mkoa tayari upo kwenye kampeni ya upandaji miti kwa kila mtoto atakayezaliwa. Pia kuanzisha mpango maalum wa kutoa chakula kwa shule za msingi na sekondari ili kuongeza ufauli.
Na mwisho amewataka wajumbe kutumia vema kikao hiko kwa kujadili mambo kadha wa kadha kwa maslahi ya watanzania na Tabora kwa ujumla.
________________
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa