Mh. Balozi Dkt Batilda Salha Burian, Mkuu wa Mkoa wa Tabora leo tarehe 30.12.2022 amefungua Mkutano mkuu wa Chama cha Ushirika wa Tumbaku WETCU (2018) LTD uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Utumishi wa Umma (Uhazili) Tabora.
Pamoja na mambo mengine Mhe Mkuu wa Mkoa
katika hotuba yake amesisitiza mambo yafuatayo;
1. Viongozi na Wanachama kuwa waadilifu na weledi katika shughuli zao za kila siku kwani uhai wa Chama unategemea Viongozi na mwanachama mmoja mmoja.
2.Kudhibiti utoroshaji wa Tumbaku, ubadhirifu wizi na matumizi mabaya ya madaraka.
3. Kuzuia kukopesha pembejeo kwa kubadilishana na mifuko ya mbolea na tumbaku.
4.Kuzuia vyama vya ushirika kupeana mikopo bila kufuata misingi ya Ushirika.
Aidha Mh. Mkuu wa Mkoa amewaeza wajumbe wa Mkutano wa 30 wa WETCU dhamira ya dhati na njema ya mh. Dkt. Samia Suluhu hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuboresha sekta ya kilimo ili iwe ya kisasa zaidi kwa kuinua tija na ubora wa mazao mbalimbali ikiwemo na zao la tumbaku.Serikali imetafuta wanunuzi wa zao la tumbaku na hii imesababisha makisio ya ongezeko la uzalishaji kutoka kilo 16,000,000 kwa msimu wa 2021/2022 hadi kilo 27,639,580 kwa msimu wa 2022/2023 sawa na ongezeko la asilimia 72.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa