Mkuu wa mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, leo tarehe 06/04/2023 amezindua mradi wa maji kata ya Usunga, wilayani Sikonge kama moja ya mkakati wa serikali wa kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi vijijini kwa asilimia 65. Mradi huo wenye thamani milioni 229.8 umesimamiwa na RUWASA, umekamilika kwa asilimia 100 na utahudumia wakazi wapatao 2038.
Mkuu wa mkoa Dkt. Batilda Burian ametoa shukrani kwa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha nyingi ambayo imetekeleza miradi mingi ya maji kwa miaka miwili ya uongozi wake.
Ametoa wito kwa wakazi wa Usunga kutunza na kuilinda miundombinu ya maji ili iwe na faida kwa wananchi wote. Sambamba na hilo kutunza vyanzo vya maji kwa upandaji wa miti.
Dkt. Batilda amewataka wakazi wa Tabora kuvuna na kuhifadhi maji ya mvua kwenye mabwawa ili kuhakikisha mkoa unakuwa na maji ya kutosha kwa shughuli za kilimo na ufugaji.
Pia amewataka wakazi wa Tabora kutambua fursa zilizopo kwenye rasilimali ya maji hususani upandaji wa miti na maua, ili kutoa fursa kwa vijana kwenye shughuli za uzalishaji mali na kuacha michezo yenye kuhusiana na bahati nasibu(Kamali).
Kupitia hadhara hiyo, Dkt. Batilda alitoa salamu za Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa waumini wa dini ya Kikristo kufuatia msimu wa sikukuu ya Pasaka.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa