• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

“WATAALAMU WA KILIMO TWENDENI TUKASIMAMIE UZALISHAJI KWA KUZINGATIA UTABIRI WA HALI YA HEWA.” DKT. MBOYA

Posted on: November 6th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, ameongoza kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa shughuli za kilimo kwa kuzingatia utabiri wa hali ya hewa uliotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kwa msimu huu wa kilimo.

Kikao hicho, kilichowakutanisha maafisa kilimo kutoka halmashauri zote za Mkoa wa Tabora na wataalamu kutoka Ofisi ya Kilimo ya Mkoa, kililenga kuweka mikakati ya kuongeza tija ya uzalishaji huku wakulima wakihimizwa kulima mazao yanayostahimili ukame kutokana na mwenendo wa mvua unaotarajiwa kuwa wa wastani hadi chini ya wastani. Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho, Dkt. Mboya aliwataka wataalamu wa kilimo kuhakikisha wanakuwa karibu na wananchi, kuwashauri kwa wakati, na kusimamia ipasavyo shughuli za uzalishaji.

 “Kuweni karibu na wananchi ili muweze kuwashauri vema wakulima wetu. Natoa wito kwa sekta binafsi na sekta za umma kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia taarifa za utabiri wa hali ya hewa, ili wananchi waweze kufanya maamuzi sahihi kwa ujasiri,” alisema Dkt. Mboya.

Kwa upande wake, Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Kanda ya Magharibi – Tabora, Waziri Omari Waziri, aliwasilisha taarifa ya utabiri wa msimu akibainisha kuwa mvua za msimu huu zinatarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani katika maeneo mengi ya Mkoa wa Tabora.

“Wananchi wanapaswa kuzingatia ushauri wa wataalamu wa kilimo na mifugo ili waweze kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza kutokana na mwenendo wa mvua,” alifafanua Waziri.

Aliongeza kuwa TMA inasisitiza wadau wote wa sekta mbalimbali kama wafugaji, mamlaka za maji, afya na wanyamapori kuendelea kutumia taarifa za hali ya hewa katika kupanga shughuli zao za kila siku.

Naye Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Kilimo, Mifugo, Uzalishaji na Ushirika, Abaraham Mndeme, alieleza kuwa kutokana na utabiri huo, halmashauri zote zimeelekezwa kuwahimiza wakulima kulima mazao yanayostahimili ukame kama vile mtama, uwele na mihogo.

“Wakurugenzi wa halmashauri wahakikishe wanawafikia wananchi na kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa kufuata ushauri wa wataalamu ili kuepuka hasara katika uzalishaji,” alisema Mndeme.

Kikao hicho kilihitimishwa kwa majadiliano ya mipango na mikakati ya utekelezaji wa shughuli za kilimo kulingana na hali ya hewa, ambapo kila halmashauri ilitakiwa kuandaa mpango wa kuelimisha wakulima na wafugaji kuhusu mbinu bora za kilimo na ufugaji endelevu.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • “WATAALAMU WA KILIMO TWENDENI TUKASIMAMIE UZALISHAJI KWA KUZINGATIA UTABIRI WA HALI YA HEWA.” DKT. MBOYA

    November 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA TABORA AONGOZA WANANCHI KUPIGA KURA, AIPONGEZA TUME HURU YA UCHAGUZI KWA MAANDALIZI MAZURI

    October 29, 2025
  • MAANDALIZI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MKOA WA TABORA YAKAMILIKA: WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUPIGA KURA, OKTOBA 29

    October 27, 2025
  • MKUU WA MKOA WA TABORA AONGOZA DUA MAALUM YA KULIOMBEA TAIFA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.

    October 24, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa