• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA HUDUMA MAALUM ZA “MADAKTARI BINGWA WA MAMA SAMIA” AWAMU YA TANO MKOA WA TABORA

Posted on: April 28th, 2025

Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Joackim Mhagama, ameongoza uzinduzi wa mpango maalum wa huduma za kibingwa kutoka kwa madaktari bingwa wa "Mama Samia Awamu ya Tano" katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Isike Mwanakiyungi. Mpango huu unaolenga kuwafikia wananchi walioko mbali na hospitali kubwa, umetajwa kuwa ishara ya ubunifu, uzalendo na upendo kwa taifa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Deusdedith Katwale alitoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Afya kwa kuleta huduma hizi muhimu. Alieleza kuwa mpango huu umesaidia wananchi wasiokuwa na uwezo wa kufuata huduma za kibingwa katika hospitali kubwa, hivyo kuokoa maisha na kuboresha afya za jamii za pembezoni.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, alieleza kuwa mkoa umehamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupata huduma hizo, akimshukuru Waziri Mhagama kwa kuleta madaktari bingwa mkoani humo. Alisisitiza kuwa ushirikiano baina ya viongozi na wataalamu wa afya utaongeza ufanisi wa huduma hizi.

Katika hotuba yake, Waziri Mhagama aliwapongeza madaktari bingwa kwa juhudi kubwa wanazozifanya nchi nzima, akibainisha kuwa mpango huu ni kipaumbele cha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Afya mwaka 2024, zaidi ya wananchi 154,015 walihudumiwa na madaktari bingwa waliotembelea halmashauri zote 184 za Tanzania Bara.

Aidha, Waziri alisifu mafanikio ya sekta ya afya katika kupunguza vifo vya akina mama wajawazito kwa asilimia 80, mafanikio yaliyowezesha Tanzania kupata tuzo ya kimataifa ya "Goalkeepers" kutoka Taasisi ya Gates. Alitoa wito kwa madaktari kuendeleza maadili ya utabibu, kuelimisha wenzao na kuhudumia wananchi  kwa moyo wa uzalendo.

Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania, Dkt. Charles Sagoe-Moses, ambaye alipongeza jitihada za serikali za kufikisha huduma bora za afya katika maeneo yenye changamoto za miundombinu, akisisitiza umuhimu wa kuendeleza juhudi hizi kwa ustawi wa wananchi.

MWISHO.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WIZARA YA AFYA NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA TABORA YAENDESHA KIKAO ELEKEZI CHA MREJESHO WA MAFUNZO NA MAPITIO YA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

    May 14, 2025
  • JESHI LA POLISI TABORA LAPATA MAGARI 6 MAPYA KWA AJILI YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

    May 12, 2025
  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa