Kufuatia kongamano la kibiahara lililofunguliwa leo Mkuu wa Hazina ndogo (M) Tabora Ndugu. Amina Said Muhomba ambaye alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa Tabora Mh. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amefungua kongamano la kibiashara la wanawake mkoani Tabora. Akiongea na wanawake waliojitokeza Ndugu. Amina Said alianza kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kwa ajili ya kuwakwamua wananawake kupitia majukwaa ya wanawake. Sambamba na hilo alitoa shukrani kwa mkuu wa mkoa wa Tabora, kwa kupata nafasi ya kumuwakilisha na kushiriki kongamano hilo.
Aidha, amewataka wanawake kuyatumia makongamano hayo kwa maendeleo ya umma. Na kwamba serikali na wadau mbalimbali wawekeza fedha nyingi ili kuhakikisha elimu ya biashara inawafikia wanawake wengi.Sambamba na hilo kwa kushirikiana na wadau, tutahakikisha tunaweka mazingira mazuri ya biashara kwa wanawake, kupitia utolewaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri zetu.Pia amewataka wanawake kutumia muda wao kutoa elimu kwa wengine kuhusiana na fursa za kibiashara zitakazopatikana kwenye kongamano hili. Na kusisitiza suala la uwajibikaji, kujituma na mshikamano miongoni mwa wanawake.
____________________________
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa