Mkuu wa mkoa wa Tabora Mh. Balozi Batilda Salha Burian leo tarehe 13/04/2023 amekutana na kuongea na wakazi wa kata ya Kigwa wilayani Uyui. Akiongea na wananchi hao, Dkt. Batilda amesema kuwa, serikali yaw amu ya sita chini ya Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi katika miradi yam aji mkoani Tabora. Na kama uongozi wa mkoa utahakikisha unasimamia fedha hizo kikamilifu ili kuhakikisha wananchi wa mkoa wa Tabora wanapata maji kwa asilimi 65 vijijini na asilimia 85 mijini.
Aidha ametoa angalizo kwa wakandarasi wanaosimamia miradi yam aji mkoani tabora, kukamilisha miradi hiyo kwa wakati ili kuhakikisha huduma za maji zinawafikia wananchi husika. Ameitaka RUWASA kuwachukulia hatua wakandarasi wote wanaochelewesha. Ametoa wito kwa wananchi kutambua kuwa serikali inafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha miradi ya maji inawafikia wananchi kwa wakati. Kupitia RUWASA mkoa wa Tabora umefanikiwa kutekeleza miradi mingi ya maji na bado mingine inazidi kutekelezwa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa