Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian alifika Wilayani Urambo kwa ajili ya ziara ya Siku moja, kukagua miradi ya Afya na Elimu, ambapo alipokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Kamishina Mwandamizi Msaidizi Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe.Elibariki Saimon Bajuta aliyeambata na baadhi ya viongozi akiwemo Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margaret Sitta.Novemba, 13, 2023
Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margaret Sitta akitoa salamu za Jimbo la Urambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian.
Akitoa salamu zake Mhe. Margaret Sitta amemshukuru Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano anaoupata kutoka kwa viongozi wote wa ngazi ya Mkoa na Wilaya katika kipindi chote tangu kufariki kwa aliyekuwa Spika Wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Samuel Sitta ambaye alifariki mwaka 2016.
Ameongeza kuwa, kupitia kumbukumbu za kifo hiko, Kila mwaka familia kwa kushirikiana na Serikali itahadhimisha siku hiyo kwa kutoa mchango mkubwa kwa wananchi, Novemba, 13, 2023
Mkuu wa Wilaya ya Urambo Kamishina Mwandamizi Msaidizi. Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe. Elibariki Saimon Bajuta akitoa salamu za Wilaya kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian mara baada ya kuwasili Wilayani hapo, Novemba, 13, 2023
Ambapo akitoa salamu zake Mhe. Bajuta ameeleza hali ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliwemo miradi ya Afya na Elimu ambayo inatarajiwa kutembelewa na Mkuu wa Mkoa.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwasili Hospitali ya Wilaya ya Urambo kukagua mradi wa ujenzi wa jengo ya Utawala, jengo la Mionzi na Jengo la Wagonjwa wa nje pamoja na jengo la Mahabara uliogharimu makisio ya Shilingi zaidi ya Bilioni 1.1 na kisha kuzindua Programu ya Madaktari Bingwa.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akisikiliza taarifa ya mradi wa ujenzi wa jengo Utawala, jengo la Mionzi na jengo la Wagonjwa wa nje pamoja na jengo la Mahabara iliyosomwa na Dkt. Gloria Dionis ambapo mpaka kukamilika kwake mradi huo utagharimu makisio ya Shilingi Bilioni 1.1 na unatarajiwa kukamilika mnamo Novemba, 18 2023.
Akisoma taarifa hiyo Gloria ameeleza malengo ya mradi huo ni kuongeza huduma ya mama na mtoto na kukuza utoaji wa huduma bora za kimahabara pamoja na huduma za upasuaji.
Aidha. Dkt. Gloria ameeleza kuwa licha ya kuwa na malengo hayo makubwa katika mradi huo, bado kuna changamoto zinazoikabili hospitali hiyo,lkama, uhaba wa nyanzo vya maji na ukosefu wa chanzo cha nishati cha uhakika.
Akihitimisha taarifa yake, Dkt. Gloria ametoa pongezi na shukrani kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutoa fedha jumla ya shilingi Milioni 900 ambazo zimekamilisha hatua kubwa ya ujenzi wa majengo hayo. Pia ametoa pongezi kwa uongozi wa Mkoa na Wilaya pamoja na Mbunge wa Jimbo la Urambo kwa kuhakikisha fedha zilizotolewa zinakamilisha mradi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora akiwasili kwenye hafla ya Uzinduzi wa Programu ya Madaktari Bingwa uliofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo. Novemba 13, 2023
Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margaret Sitta akitoa neno la shukrani kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian baada ya ufunguzi wa Programu ya Madaktari bingwa uliofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo. Novemba 13, 2023
Kamishina Mwandamizi Msaidizi. Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe.Elibariki Saimon Bajuta akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian kwenye tukio la kukata utepe na kisha kuhutubia wananchi waliofika kwenye hafla ya uzinduzi wa Programu ya Madaktari Bingwa iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo.
Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akikata utepe kuashiria kuwa uzinduzi wa Programu ya Madaktari bingwa umekamilika, wengineo ni Mkuu wa Wilaya ya Urambo Kamishina Mwandamizi Msaidizi. Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe.Elibariki Saimon Bajuta, Mbunge wa Jimbo la Urambo Margaret Sitta, Katibu Tawaa (W) Urambo Ndugu. Innocent Nsena na Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Ndugu. Grace Quintine.
Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akihutubia wananchi waliofika kwenye hafla ya Uzinduzi wa Programu ya Madaktari Bingwa ilifanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo.
Ambapo kwenye hotuba yake, Mhe. Mkuu wa Mkoa ameeleza mafanikio makubwa katika sekta ya afya kwa kipindi cha miaka mwili ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ambapo kumejengwa hospitali za Wilaya zaidi ya tako (5) tofauti na hapo awali hospitali zilikuwa mbili mkoa mzima.
Aidha ameelezea maboresho makubwa kwenye hospitali zetu hususani ujenzi wa majengo ya Dharula (EDM, majengo ya maabara, majengo ya mionzi na majengo ya Wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU)
Ametoa wito kwa Wakurugenzi kuanza michakato ya kuandaa fedha kwa ajili ya manunuzi ya vifaa tiba ili kuhakikisha kila zahanati inapokamilika inakuwa na vifaa tiba, kwani tayari Serikali imeshatoa fedha.
Aidha Mhe. Batilda ametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa hii ya madaktari bingwa, kwani huduma hizi zina gharama kama ukizipata nje ya programu hii. Na pia amewataka wananchi wa Urambo kuendeleza utamaduni wa kufanya mazoezi ili kuimarisha afya ya mwili.
Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Kamishina Mwandamizi Msaidizi. Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe.Elibariki Saimon Bajuta, Mbunge wa Jimbo la Urambo Margaret Sitta, Katibu Tawaa (W) Urambo Ndugu. Innocent Nsena na Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Ndugu. Grace Quintine Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Mhe. Adamu Malunkwi pamoja na madaktari bingwa.
Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Kamishina Mwandamizi Msaidizi. Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe.Elibariki Saimon Bajuta, Mbunge wa Jimbo la Urambo Margaret Sitta, Katibu Tawaa (W) Urambo Ndugu. Innocent Nsena na Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Ndugu. Grace Quintine Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Mhe. Adamu Malunkwi pamoja na Kamati ya Usalama (W) Urambo.
Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Kamishina Mwandamizi Msaidizi. Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe.Elibariki Saimon Bajuta, Mbunge wa Jimbo la Urambo Margaret Sitta, Katibu Tawaa (W) Urambo Ndugu. Innocent Nsena na Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Ndugu. Grace Quintine Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Mhe. Adamu Malunkwi pamoja na Wananchi waliofika kwenye hafla ya uzinduzi wa programu ya Madaktari Bingwa.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda ametembelea na kufanya mazungumzo katika ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Urambo na kukutana na baadhi ya viongozi na wanachama wa CCM. Mkuu wa Mkoa aliambata na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Kamishina Mwandamizi Msaidizi. Mamlaka ya Uhifadhi. Mhe. Elibariki Saimon Bajuta pamoja na Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margaret Sitta
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Buria ametembelea kituo cha Afya cha Vumilia kilichopo Kata ya Vumilia, Wilaya ya Urambo ambapo Mkuu wa Mkoa amerishwa utekelezaji wa mradi huo ambao bado ujenzi wake unaendelea.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian ikiwa Wilayani Urambo alitembelea mradi wa ujenzi wa majengo manne yaliopo katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo, Alizindua Program ya Madaktari Bingwa, alitembelea ofisi za Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Urambo na mwisho alitembelea Mradi wa Kituo cha Afya za Vumilia.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa