Wananchi Mkoani Tabora wametakiwa kuchangamkia fursa za Masomo yanayotolewa na Chuo cha madini Nzega Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo hiki Nuru Msengese amesema inasikitisha kuona hakuna mwanafunzi hata mmoja ambaye anatoka Mkoa wa Tabora aliyejiunga na Chuo hicho Mwaka wa Masomo 2023.
Msengema ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa Kwanza na kuongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa Chuo hicho miaka mitatu iliyopita bado kiasi cha udahili kwa wanafunzi wanaotoka Mkoa wa Tabora ni ndogo ikilinganishwa na wale wanaotoka katika Mikoa mingine.
Afisa Tarafa wa Nyasa Wilaya ya Nzega Ricardo Komanya anasema kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Elimu wataongeza mbinu katika kukitangaza chuo hicho kwa wananchi ili kiweze kudahili wanafunzi wengi zaidi wakiwemo wa kutoka Mkoa wa Tabora.
Ameongeza kuwa ni heshima kubwa kwa Wilaya ya Nzega kuwa na Tawi la Chuo cha Madini, Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa