• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA, KILIMO NA MIFUGO YARIDHISHWA NA UJENZI WA JENGO LA BODI YA TUMBAKU KANDA YA MAGHARIBI MKOA WA TABORA

Posted on: March 16th, 2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini imetembelea na kukagua  mradi wa ujenzi wa jengo la Bodi ya Tumbaku Kanda ya Magharibi, unaojengwa katika mkoa wa Tabora kwa gharama ya shilingi bilioni 1.23.

Mhe. Mwanyika ameipongeza Bodi ya Tumbaku kwa kuanzisha mradi huu muhimu, ambao utasaidia katika usimamizi wa zao la tumbaku na kutoa mchango mkubwa katika mapato ya serikali kupitia upangishaji wa sehemu ya jengo hilo kwa matumizi ya kibiashara.

Wajumbe wa kamati hiyo, licha ya kubaini kasoro chache katika utekelezaji wa mradi huo, walionesha kuridhika na ubora wa kazi inayofanywa hadi sasa. Walitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku, Ndg. Stanley Mnozya, kuhakikisha kwamba changamoto zilizojitokeza zinatatuliwa kwa haraka na kwa  ufanisi.

Akihitimisha kikao cha majumuisho, Mhe. Mwanyika alisisitiza umuhimu wa usimamizi makini na wa kitaalamu katika kazi za ujenzi wa miradi ya umma, kuanzia hatua za awali hadi mwisho. Aliipongeza Bodi ya Tumbaku kwa mabadiliko ya kimkakati yaliyofanywa kwenye mradi huo, ambapo jengo hilo litakuwa kitega uchumi, jambo litakalosaidia kuongeza faida kwa taasisi hiyo.

Aidha, Mhe. Mwanyika alitoa maelekezo kwa mkandarasi wa mradi huo, Suma JKT, kuhakikisha kuwa anakamilisha kazi kwa weledi na ubora wa hali ya juu, na kwamba mradi huo ukamilike kwa wakati.

Kwa upande wake, Ndg. Victor Mwambalaswa, Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Tanzania, kwa niaba ya bodi hiyo, aliishukuru Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo kwa kutembelea mradi huo na kutoa maelekezo ya muhimu ya kisekta. Ameihakikishia kuwa maelekezo yote yaliyotolewa yatazingatiwa na kufanyiwa kazi ili kuboresha utekelezaji wa mradi kwa ufanisi.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa