• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MHE. CHACHA, AFANYA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, HUKU AKISIMAMIA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WANAOSHINDWA KUSIMAMIA WELEDI.

Posted on: February 18th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Matiko Chacha, amefanya ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika Wilaya ya Tabora na Nzega. Katika ziara hiyo, Mhe. Chacha alikutana na watumishi wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) pamoja na wale wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Katika hatua muhimu, Mhe. Chacha alimsimamisha kazi Meneja wa GPSA Mkoa wa Tabora, Bw. Mayala Mbuli, ili kupisha uchunguzi zaidi kuhusu tuhuma zinazomkabili za utovu wa nidhamu na kushindwa kutoa huduma bora kwa wateja. Aidha, alimuagiza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tabora, Mhandisi Raphael Mlimaji, kuchukua hatua dhidi ya watumishi wawili wa TANROADS kwa tuhuma za kupokea rushwa katika mzani mdogo wa Tuli.

Ziara ya Mhe. Chacha ilikamilika wilayani Nzega, ambapo alitembelea machimbo ya dhahabu katika Kijiji cha Isanga, Kata ya Lusu. Akiwa huko, aliwashauri wananchi kuwa makini na matapeli wanaotumia hadaa kuwadanganya viongozi wa serikali na wananchi kwa manufaa yao binafsi. Mhe. Chacha alimpongeza Bi. Rehema Salim, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji wa Dhahabu cha Mkombozi, kwa ujasiri wake wa kutoa taarifa kuhusu matapeli waliovamia eneo la wachimbaji na kuanza kuchimba dhahabu kinyume cha sheria.

Vilevile, Mhe. Chacha alimuamuru Mkuu wa Chuo cha Madini Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bw. Abrahamu Lwakajunguti, kuondoka mara moja katika eneo hilo kwa tuhuma za kuruhusu wachimbaji kuingia katika eneo la chuo hicho na kuchimba dhahabu kinyume cha sheria. Pamoja na kuonesha utovu wa nidhamu kwa viongozi pamoja na wananchi wa eneo hilo.

Ziara ya Mhe. Chacha ilihitimishwa kwa agizo la kumaliza mgogoro kati ya Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya Savanna Reef na mchimbaji mdogo wa madini, Bw. Nshishi. Alisisitiza kuwa mgogoro huo hauwezi kufaidisha pande yoyote na unadumaza tu shughuli za uzalishaji katika eneo hilo, hivyo alitoa agizo la kumaliza tofauti hizo haraka.

 Ziara hii inadhihirisha juhudi za Mhe. Chacha katika kutatua changamoto za wananchi na kuhamasisha uwajibikaji katika taasisi za umma na sekta ya uchimbaji madini.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa