Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Paulo Chacha, ameungana na wakuu wa mikoa wengine katika mkutano wa uhamasishaji wa ukuzaji na uendelezaji wa shoroba za kilimo uliofanyika tarehe 12 Februari 2026 mkoani Singida.
Mkutano huo ulilenga kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika kukuza sekta ya kilimo, kuongeza tija katika uzalishaji na kuchochea maendeleo ya uchumi wa Taifa kupitia matumizi bora ya rasilimali zilizopo katika mikoa husika.
Kikao hicho kiliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, na kilihusisha viongozi na wataalamu kutoka mikoa ya Shinyanga, Tabora na Dodoma. Miongoni mwa washiriki walikuwa Makatibu Tawala wa mikoa hiyo, wataalamu wa kilimo pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo nchini.
Washiriki walijadili mikakati ya pamoja ya kuendeleza shoroba za kilimo, kuboresha miundombinu ya uzalishaji na masoko, pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika mnyororo mzima wa thamani wa mazao ya kimkakati.
Hatua hiyo inaelezwa kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kuifanya sekta ya kilimo kuwa injini ya ukuaji wa uchumi na chanzo kikuu cha ajira na kipato kwa wananchi.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa