• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

Posted on: July 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Matiko Chacha, amewaongoza viongozi wa mkoa huo kuwapokea kwa shangwe wanamichezo waliouwakilisha mkoa katika mashindano ya UMISSETA ngazi ya Taifa yaliyofanyika mkoani Iringa kuanzia Juni 20 hadi 29, 2025.

Katika hafla hiyo maalum ya mapokezi, Mhe. Chacha aliwapongeza wanamichezo hao kwa ushindi mkubwa walioupata, ambapo Tabora ilishika nafasi ya tatu kitaifa kwa kupata alama 178.6, pamoja na kuibuka mabingwa wa kwanza kitaifa katika mchezo wa riadha.

Kwa upande wake, Afisa Elimu wa Mkoa wa Tabora, Mwalimu Upendo Ulaya, aliwashukuru kwa dhati viongozi wa serikali  mkoa na wadau wote waliowezesha maandalizi ya timu hiyo. Alieleza kuwa, kwa mafanikio haya, tayari kuna mpango kabambe wa kuanzisha vitalu vya kuandaa vipaji vya  wanamichezo mahiri kwa ajili ya mashindano umitashumta na umisseta kwa msimu ujao.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, hakubaki nyuma katika kupongeza juhudi hizo, akieleza kuwa ushindi huo ni matokeo ya kazi kubwa iliyofanywa na wachezaji, walimu na viongozi. “Ni fahari kwa Tabora, na ushindi huu umeendelea kutubakiza katika ramani ya michezo kitaifa. Endeleeni kuwa na nidhamu na kumcha Mungu katika kila hatua ya maisha yenu,” alisisitiza Dkt. Mboya.

Katika kuthamini mchango wa wanamichezo hao, Mhe. Chacha alikabidhi vyeti vya pongezi na zawadi kwa wachezaji na walimu wao, huku akidhamiria kuanza mchakato wa kuwachagua na kuwaendeleza vijana wenye umri chini ya miaka 17 watakaoweza kujiunga na timu za mkoa katika michezo mbalimbali.

Mashindano ya UMISSETA mwaka huu yaliandaliwa chini ya kaulimbiu: “Viongozi Bora ni Msingi wa Maendeleo ya Taaluma, Sanaa na Michezo — Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu.” Kaulimbiu hiyo ililenga kuhimiza ushiriki wa vijana katika maendeleo ya kitaifa kupitia taaluma na michezo sambamba na kuhamasisha mshikamano wakati wa uchaguzi mkuu ujao.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa