• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

BARAZA LA USHAURI MKOA WA TABORA LAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 367.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

Posted on: March 6th, 2025

Mkuu wa wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai, ameongoza baraza la ushauri la mkoa (RCC) katika ukumbi wa mikutano wa Isike Mwanakiyungi, uliopo manispaa ya Tabora, kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha. Katika kikao hicho, katibu Tawala msaidizi, mipango na uratibu, Bw. Asanterabi Sang’enoi, aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mpango wa bajeti ya mwaka 2024/25 na mapendekezo ya bajeti kwa mwaka 2025/26.

Bw. Sang’enoi alisema kuwa, mkoa wa Tabora uliidhinishiwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kiasi cha shilingi bilioni 325.8, ambapo shilingi bilioni 314.5 ni kwa bajeti ya halmashauri, na shilingi bilioni 11.7 ni bajeti ya sekretarieti ya mkoa. Kwa mwaka wa fedha 2025/26, mkoa wa Tabora umepanga kutumia kiasi cha shilingi bilioni 367.2 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa huo.

Wajumbe wa mkutano huo walikubaliana kwa pamoja kupitisha rasimu ya bajeti ya mwaka 2025/26 na walipendekeza marekebisho yafanyike, hasa katika eneo la ununuzi wa magari ya viongozi na ujenzi wa ofisi za wakuu wa wilaya, maeneo ambayo walitaka yapatiwe kipaumbele.

Akichagia mjadala huo, Katibu Tawala wa mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia maelekezo mahususi katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka ujao. Alisema kuwa, ni muhimu kuepuka kuanzisha miradi mipya ya maendeleo kabla ya kumaliza miradi iliyopo. Aidha, alisisitiza kuwa ujenzi na uanzishwaji wa miradi ya maendeleo unategemea miongozo ya kitaalam kutoka katika wizara, na siyo matakwa ya viongozi wala wataalam wa maeneo husika.

Mwenyekiti wa kikao hicho, Mhe. Tukai, alitoa rai kwa viongozi na wananchi wa Tabora kushirikiana katika kutokomeza vitendo vya ukatili, ambao vimekuwa vikishamiri katika mkoa huu na hii ni kwa  mujibu wa takwimu zilizowasilishwa na afisa ustawi wa jamii. Alihamasisha kuwa, kwa kushikamana, vitendo vya ukatili wa kijinsia vitakuwa historia katika mkoa wa Tabora.

Akifunga kikao hicho, Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Tabora, Ndg. Mohamed Nassoro Hamdan (MNEC), alishukuru kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Tabora, ikiongozwa na Mhe. Paul Chacha, kwa kazi nzuri ya kudumisha amani na utulivu. Alitoa wito kwa wananchi kuendelea kuitunza na kuidumisha amani hiyo, akisisitiza kuwa hakuna miradi ya maendeleo itakayoweza kuendeshwa  wala kutekelezwa bila amani.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa