• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

"UWAJIBIKAJI NA USALAMA KWANZA: PPRA KANDA YA MAGHARIBI NA KATI YAFANYA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI NA KUTOA MAFUNZO YA KUKABILI MAJANGA YA MOTO TABORA"

Posted on: July 8th, 2025

Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kanda ya Magharibi na Kati, Bi. Suma Atupele, ameongoza kikao cha tathmini ya utendaji kazi kwa mwaka 2024/2025 na kuwasilisha mpango kazi wa mwaka ujao wa 2025/2026, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Bevac, ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Bi. Atupele amewataka wataalamu wa ununuzi wa umma kuwa wabunifu na kufanya kazi kwa bidii kubwa ili kufanikisha matarajio ya Serikali katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Amebainisha kuwa mafanikio katika sekta ya ununuzi wa umma yanategemea sana weledi, uwajibikaji na ufuatiliaji wa karibu wa shughuli zinazotekelezwa na taasisi za umma.

"Ni muhimu kuandaa na kuwasilisha mpango wa mafunzo kazini kwa wakati, huku tukizingatia uhalisia wa bajeti na utekelezaji wake ili kuongeza ufanisi na tija kazini," alisisitiza Bi. Atupele.

Ameongeza kuwa lengo la kuanzishwa kwa ofisi za kanda za PPRA ni kusogeza huduma karibu na wananchi na kufanya ukaguzi wenye tija unaolenga kuzuia upotevu, ubadhirifu na uharibifu wa fedha za umma katika utekelezaji wa shughuli za ununuzi kwenye taasisi za serikali.

“Ukaguzi tunaoufanya una lengo mahsusi la kuhakikisha kuwa fedha za Serikali zinatumika kwa uadilifu mkubwa na kwa manufaa ya wananchi,” alifafanua Meneja huyo.

Kikao hicho pia kiliambatana na mafunzo maalum juu ya majanga ya moto na ukoaji, yaliyoratibiwa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tabora. Mafunzo hayo yaliongozwa na Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi hilo, Bi. Teresia Kipete, kwa kushirikiana na Koplo Stephano Kombo na S/Sgt Mayasa Choka.

Watumishi wa PPRA walipewa elimu juu ya aina za moto, visababishi vya ajali za moto, mbinu za kuzuia majanga hayo, pamoja na hatua za kuchukua pindi moto unapozuka katika majengo ya ofisi na makazi. Maafisa hao wamesisitiza umuhimu wa kuwa na vifaa vya kuzimia moto, kufunga ving’amua moto katika ofisi, kuwa na maeneo ya dharura ya mkusanyiko na mpango madhubuti wa kujinusuru wakati wa majanga.

Mafunzo hayo yamekusudia kuwajengea uwezo watumishi wa PPRA kanda ya Magharibi na Kati ili waweze kuchukua tahadhari na hatua stahiki kwa usalama wa maisha na mali pale wanapotekeleza majukumu yao ya kila.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • "UWAJIBIKAJI NA USALAMA KWANZA: PPRA KANDA YA MAGHARIBI NA KATI YAFANYA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI NA KUTOA MAFUNZO YA KUKABILI MAJANGA YA MOTO TABORA"

    July 08, 2025
  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa