BASHE AAGIZA COASCO KUTAAFUTA MBINU KUJITEGEMEA
NAIBU Waziri wa Kilimo Hussein Bashe ameliagiza Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) kutafuta mbinu ya kupata vyanzo vyao vya mapato vya kuendesha shughuli za kiukaguzi ili wawe uhuru.
Alisema kitendo cha kutegemea ada za ukaguzi kutoka Vyama vya Ushirika vinawafanya kutoka kuwa uhuru wakatika kuendesha shughuli za ukaguzi
Bashe alitoa kauli hiyo leo wakati wa kutembelea mabanda mbalimbali ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za siku ya Ushirika Duniani (SUD) ambapo Kitaifa inafanyika Mkoani Tabora na kilele kitakuwa tarehe 3 Julai mwaka huu.
Kwa uande wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COASCO Zavery Mkingule alisema wakipewa kiasi cha shilingi bilioni 4 kwenye fedha za Matumizi ya Kawaida kwenye bajeti yao wataweza kufanya kazi bila vikwazo.
Alisema hivi sasa wanaata kiasi cha shilingi bilioni 1 ambazo haziwatoshi kuwatuma wakaguzi kwenda kukagua vyama mbalimbali kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.
Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani mwaka huu ni Ushirika pamoja tujijenge uya kwa ubora na tija.
MWISHO
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa