Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amemshukuru Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha Bilioni 257 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya maji Mkoani Tabora ambayo imeongeza hali ya upatikanaji wa maji. Ameyasema hayo leo Oktoba 13, 2023 alipokuwa akifungua Kikao cha Mrejesho wa Utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa bwawa la Igombe, kilichofanyika katika Ukumbi wa Chuo Cha Ualimu (TTC) Manispaa ya Tabora.
“Namshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia Zaidi ya Bilioni 257 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji na kuongeza hali ya upatikanaji wa maji asilimi 75 kwa mijini na asilimia 68 kwa vijijini”
Sambamba amewashukuru na kuwapongeza watendaji wote wa Taasisi ya Bonde la Ziwa Tanganyika kwa utendaji uliotukuka na kuwataka watendaji hao kuendeleza juhudi na kasi ya kurinda na kuthibiti uharibifu na uchafunzi wa vyanzo vya maji.
“Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru watendaji wote wa Taasisi ya Bonde la Ziwa Tanganyika kwa utendaji wao uliotukuka na nitoe wito kwao kuongeza kasi ya kulinda na kudhibiti uharibifu na uchafuzi wa vyanzo vya maji” Alisistiza Mku wa Mkoa
Aidha Mkuu wa Mkoa amebainisha changamoto zilizokuwa zinalikabili Bwawa la Igombe zikiwemo kuzeeka kwa tuta, kujaa tope na mchanga sambamba na ulishaji na uchungaji wa mifugo, na kwamba ameridhishwa na ukarabati uliofanywa ambao umepunguza changamoto hizo kwa kiasi kikubwa.
“kwa hakika nimeridhishwa sana na ukarabati uliofanywa ambao umetatua baadhi ya changamoto ambazo zilikuwa zinalikabili bwawa hili, changamoto kama kuzeeka kwa kuta za bwawa, kujaa mchanga na tope sambamba na shughuli za kibinadamu hususani ufugaji” alisema Dkt. Batilda.
Itakumbukwa kuwa, mnamo mwezi Mei, kulifanyika kikao cha uwasilishwaji wa changamoto ambazo zinalikumba Bwawa la Igombe na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo, ambapo Serikali kupitia Wizara ya Maji, ilitenga jumla ya shilingi Bilioni 1.5 ambazo zimetumika katika ukarabati wa Bwawa hilo. Hivyo ufunguzi wa Kikao hiki ni nafasi ya kujadili na kutathimini ukarabati uliofanywa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa