Bweni la wavulana lililopo katika Shule ya Sekondari Ziba lateketea kwa Moto, alfajiri ya Januari 23, 2024 mwaka huu, ambapo Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Dk. John Mboya Kunenge amefika Shuleni hapo kujionea hali halisi ya janga hilo.
Ameeleza, Vitu ikiwemo Sare, mabegi, sabuni, na baadhi ya madaftari walivyokuwa wakikaa navyo kwenye Bweni ndivyo vimeteketea kwa moto pasipo kuacha vifo wala majeruhi.
"Nichukue nafasi hii kuutarifu umma tumepata Changamoto ya tukio la Moto katika Shule yetu hii ya Sekondari Ziba, tunamshukuru Mwenyezi Mungu hatukupata Madhara yanayohusisha athari za kifya na maisha ya wototo wetu,wakiwa katika nyumba ya ibada msikitini "Ameeleza Dkt. Mboya
Hata hivyo ,Ameeleza kuwa mpaka sasa Serikali ngazi ya mkoa imeshaunda tume ili kuchunguza chanzo cha moto huo na kutoa wito kwa walimu na wanafunzi kushirikiana na tume hiyo ili kubaini ukweli.
Aidha Dkt. Mboya amelishukuru Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani hapo kwa kuchukua hatua za hataka na kufanikisa kuuzima moto huo kabla ya kupeleka maafa zaidi sambamba na utoaji wa Elimu kwa Shule za Mkoa huo katika kudhibiti majanga ya moto.
Katibu Tawala John Mboya ametoa Rai kwa Shule zote za Mkoa huo kupata Mafunzo hayo ya Elimu jinsi ya kuthibiti madhara ya moto hatua za awali,kwenye hatua ya Ujenzi vitu gani viandaliwe, na endapo moto unatokea nini cha kufanya.
Nae Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tabora (SAFC) Mohammed Jihadi ameeleza kuwa moto huo ulizuka mnamo Asubuhi ya Leo saa 2: 50 ambapo Jeshi la Zimamoto Wilaya ya Igunga kwa kushirikiana na Jeshi la Zimamoto Wilaya ya Nzega walifanikiwa kudhibiti moto huo mapema na kuepusha madhara. Ameeleza kutokana na Changamoto ya moto mashuleni wapo kwenye Program ya utoaji mafunzo kwa shule ya msingi na sekondary Mkoani hapo
Kwa upande wake, Mkuu wa shule ya Sekondari Mwalimu Ally Nohoye ameeleza kuwa Bweni lililoathirika ni la wavulana na vifaa vya wavulana ndiyo vimeteketea vyote. Na tunalishukuru Jeshi la Zimamoto kwa kufika mapema na kuzuia moto huo ambao ungeweza kusambaa zaidi.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa