JESHI la Zimamoto na Ukoaji nchini limeziomba Mamlaka zinazohusika na usambazaji Maji katika maeneo mbalimbali ya wananchi hapa nchini kuhakikisha wajenga visima mitaani ili kuliwezesha kupata maji kwa urahisi ya kukabiliana na majanga ya moto yanapotokea.
Kauli hiyo imetolewa na Kamshna Jenerali wa Jeshi na Uokoaji nchini (CGF) John Masunga wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani Tabora ya kukugua shughuli za Jeshi hilo.
Alisema visima vya maji vinapokuwa maeneo ya mbalimbali na wakati mwingine katika mazingira yasiyofikika na magari yanasababisha zoezi la kuzima moto unapotokea kuwa gumu.
Kamnishna Jenerali huyo wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji aliongeza kuwa katika kukabiliana na upungufu wa magari wameingia makubaliano na Shirika la Nyumbu ambalo ni la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) la kuwatengenezea magari ya kuzimia moto.
CGF Masunga alisema magari hayo yanatarajiwa kukamilika katika muda mfupi ujao na kuongeza kuwa yatakapokamilika watayasambaza kwenye mikoa mbalimbali ili yaweze kusaidia kuongeza vitendea kazi.
Aidha Kamnishna Jenerali huyo wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji alitoa kwa jamii kutoa taarifa mapema kwa Jeshi hilo pindi wanakabiliwa na majanga ya moto, barabarani, majini na mengine ili waweze kupata msaada.
Katika hatua nyingine alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kulipatia Jeshi hilo shilingi Bilioni 5 kwa ajili ya ujenzi wa magari ya Askari wa Jeshi hilo.
CGF alisema zoezi la ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari wa Jeshi hilo umeanza na wameanzia mkoani Dodoma ambapo kumekuwepo na ongezeko kubwa la Askari kwa sababu ya kuhamia makao makuu ya nchi.
Aliongeza kwa upande wa makazi ya Askari wa Mikoani amewaagiza Makamanda wa Mikoa yote kuhakikisha wanaongea na Halmashauri kwa ajili ya kupata viwanja vya ujenzi wa nyumba za makazi ya askari.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Philemon Sengati alilishukuru Jeshi hilo Mkoani humo kwa juhudi zake za kukabiliana na majanga mbalimbali.
Alisema Ofisi yake itaendelea kushirikiana na Jeshi hilo katika kuhakikisha linazuia na kukabiliana na majanga yanapotokea
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa