Chama cha msingi cha Chimbuko (Chimbuko Amcos) kilichopo Kata ya Igagala, wilayani Kaliua, mkoani Tabora kimepanga kuzalisha zao la tumbaku kilo milioni moja (1,000,000) sawa na tani elfu moja (1000) msimu huu wa 2023/2024 ikiwa ni moja ya ishara ya kuunga mkono Serikali ya awamu ya sita inayongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha sekta ya kilimo inawakwamua wakuliwa wake. Hayo yamejiri wakati wa mkutano mkuu wa chama hiko uliofanyika Februari 27, 2024
Akisoma taarifa ya chama hiko, mwenyekiti wa Chimbuko Amcos Ndugu. Mbaga Ally Mpale amesema kuwa, kwa msimu huu wa 2023/2024 watazalisha tani 1000, ambapo kumekuwa na ongezeko la uzalishaji ukilinganisha na msimu ulipita (2023/2024) ambapo walizalisha tani 980.
Ndugu. Mbaga amesema kuwa, wamepanga kuzalisha tani 1500 kwa msimu wa 2024/2025 na hii ni kutokana na mabadiliko makubwa yaliofanywa na serikali katika kilimo cha tumbaku hususani utolewaji wa mbolea ya ruzuku ambayo imesaidia kuongeza uzalishaji kwenye kilimo hiko.
Aidha. Mwenyekiti Mbaga ameiomba Kampuni ya JTI inayohusika na ununuzi wa tumbaki katika chama hiko, kuongeza kasi ya masomo ili kuwapa nafasi wakulima kufanya maandalizi mapema ya misimu inayofuata kwa kuwa maandalizi hayo huambatana na malipo baada ya masoko kukamilika.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa