Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Mhe. Dkt Rashid Chuachua amewataka wanaushirika wote nchini kutumia makongamano ambayo Serikali na wadau wake wanayaanzisha kwa lengo la kukuza na kuendeleza Ushirika hapa nchini. Ameyasema hayo leo June 30, 2023 akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian katika Ufungaji wa Kongamano Kuu la Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yanayoendelea kufanyika viwanja vya Nanenane, Manispaa ya Tabora.
Dkt. Chuachua ameeleza kuwa “dhamira ya Serikali ya awamu ya sita ni kuona Ushirika unakua kwa maendelo endelevu katika shughuli za kiuchumi na jamii” na kusisitiza kuwa kupitia makongamano hayo wanaushirika watafaidika kwa kupata elimu na fursa mbalimbali.
Aidha Dc Chuachua ameweka wazi kuwa, Serikali inatambua mchango wa Wanaushirika katika kukuza uchumi wa taifa. “leo mmedhinilisna kuwa Ushirika ni sekta mtambuka yenye kusimamia uchumi wa nchi na kuongeza pato la taifa na kukuza uchumi wa mwanachama mmoja mmoja” alisema Dkt. Chuachua.
Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yatarajiwa kuhitimishwa kesho Julai 1, 2023 na mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe(MB).
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa