• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

DC MWANSASU : “MKAZITUMIE VIZURI PIKIPIKI HIZI"

Posted on: September 25th, 2023

Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Zakaria Mwansasu amewataka maafisa nyuki wa Wilaya kuzitumia vizuri pikipiki ambazo wamekabidhiwa leo Septemba 25, 2023,  kwenye hafla ya kukabidhi pikipiki mpya 15 zenye thamani ya shilingi milioni 131, fedha kutoka Mradi wa Kuboresha Mnyororo wa Thamani ya Ufugaji Nyuki (BEVAC) 

 

"Nawaelekeza maafisa mnaopewa pikipiki hizi mkazitumie vizuri kwa kuhakikisha zinatumika kutimiza majukumu yaliyopangwa kuboresha shuhuliza za ufugaji nyuki na siyo vinginevyo”  alisema DC Mwansasu

 

DC. Mwansasu ameleza kuwa, Serikali na wadau wake wanatambua mchango na thamani ya shughuli za ufugaji wa Nyuki ambao kila siku umekuwa na tija kubwa kwa wakazi wa Mkoa wa Tabora.

 

“Serikali inatambua umuhimu wa shughuli za ufugaji nyuki katika kutoa fursa za kiuchumi kwa wanajamii wengi hasa vijana na wakina mama. Hivyo kupitia pikipiki hizi tunaamini maafisa hawa  wataweza kusaidia kuongeza tija ya uzalishaji, uboreshaji wa mnyororo wa thamani na kupelekea kuongezeka kwa mapato katika halmashauri zetu” Alisisitiza Mhe. Mwansasu.

Sambamba na hilo Mhe. Mwansasu ameeleza baadhi ya mabadiliko ambayo yanaendelea kufanyika ili kuhakikisha shughuli za ufugaji wa Nyuki zinakwenda na wakati ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi tofauti na hapo awali.

“Kwa sasa takribani mizinga 560,000 inayotumika na wafugaji katika maendeo yautekelezaji wa mradi ni mizinga ya Asili (84%) na mizinga ya kisasa ni 110,000 tu (16%). Napenda kuyasema haya ambayo ni baadhi tu ya mambo muhimu ya kuzingatia ili kuendana na kasi ya teknologia iliyopo sasa, kwani ufugaji Nyuki wa sasa siyo ule wa mazoea kama walivyokuwa wanafanya mababu zetu” 

 

Kwa miaka ya hivi karibuni Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, shughuli za ufugaji Nyuki hasa kwa Mkoa wa Tabora umehimarika sana na hii ilipelekea Asali kutoa Tabora kupata hati ya utambuzi wa Kitamaifa huko nchini Afrika Kusini. Hali hii imechangia kuhimiza wadau wa shughuli za ufugaji Nyuki kuunga mkono shughuli hizo na kufanya mabadiliko makubwa sana.

 

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa