“Mwanasheria anapaswa na anashauriwa kujitathimini kama shauri lililo mbele yake kama atafauru au la na kuishauri halmashauri mapema kuchukua hatua stahiki kwa maslahi ya halmashauri na upande mwingine” alisema Dkt. Mboya.
Dkt. Mboya amewataka wanasheria kuangalia gharama ambazo halmashauri inaweza kuzitumia kwenye mashauri mbalimbali kabla ya kuingia kwenye mashauri yanayoikabiri halmashauri husika ili kuepukana na matumizi ya gharama kubwa kwenye shauri.
“hakikisha unatathmini kiasi cha fedha kitakachotumika kuendesha shauri ikiwemo gharama za kufungua kesi, kulipa mashahidi endapo watatoka nje ya mamlaka unayofanyia kazi” alisema Katibu Tawala
Aidha, Dkt. Mboya amewapongeza wanasheria wa mamlaka zote za serikali za kitaa mkoani Tabora kwa kushiriki kikao hiko ambacho kwa hakika kinakwenda kujenga umahiri kwa wanasheria hao na kutoa wito kwa wanasheria hao kutumia kikao hiko katika kukuza utendaji kazi katika mamlaka zao ili kuboresha huduma za kisheria kwa wananchi wa mkoa wa Tabora.
Naye, Mkuu wa Kitengo cha Sheria Mkoa wa Tabora Wakili wa Serikali Silinde Gumada amemuhakikishia Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora kuyafanyia kazi maelekezo na mapendekezo yote ambayo ameyatoa katika hotuba yake, na kwamba yeye kama mkuu wa kitengo atahakikisha maelekezo na mapendekezo yaliotolewa yanawafikia wanasheria wote kwenye mamlaka zote za serikali za mkoa wa Tabora.
Kikao cha Wanasheria Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa Mkoa Wa Tabora kilifunguliwa januari 29, 2024 na kinatarajiwa kufungwa Februari 2, 2024, ambacho kimehusisha wanasheria wote wa mamlaka zote za serikali kutoka halamashauri zote za Mkoa wa Tabora.
Na mara baada ya kumaliza Hotuba yake Dkt. John Mboya alipata nafasi ya kutoa somo kwa wanasheria hao kuhusiana na Sera ya Public Private Partnership (PPP).
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa