NA TIGANYA VINCENT
Mkurugenzi wa Mashtaka Sylvester Mwakitalu ameuomba Uongozi wa Mkoa wa Tabora kuwasaidia upatikanaji viwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi kwa kila Wilaya.
Alisema lengo ni kutaka kusogeza karibu huduma kwa wananchi.
Mkurugenzi wa Mashtaka Mwakitalu ametoa kauli hiyo leo alipofika Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa ajili kusaini vitabu vya kabla ya kuendelea majukumu mengine.
Alisema kuwa hivi wanayo Ofisi katika Wilaya ya Nzega na katika Wilaya ya Tabora wanapanga katika Jengo la Bemki ya NBC jambo ambalo linawaongezea gharama katika uendeshaji wa majukumu.
“Mheshimiwa Mkuu tunakuomba utusaidie kuwa na Viwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi zetu katika kila Wilaya…hivi sisi tuna ofisi za Mkuu wa Mashitaka katika kila Mkoa kilichobaki ni kupata katika kila Wilaya” alisema.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani amemwakikishia DPP kutafuta viwanja vya kujenga Ofisi zao kila Wilaya ili huduma kwa wananchi iwe karibu.
Alisema Ofisi ni muhimu katika kuusaidia uongozi wa Mkoa wa Tabora kukabiliana na kuyatafutia ufumbuzi matatizo na vitendo vya kiharifu kama vile vya uchomaji moto ovyo mistu na kupoteza raslimali ambazo ni muhimu katika uzalishaji wa asali.
Aidha Balozi Dkt. Batilda alisema Mkoa huo unakabiliwa na migogoro mingi ya ardhi na mirathi
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa