Kwa niaba ya wananchi wa Tabora, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, amempongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) sambamba na utiaji saini wa Hati za makubaliano 14 na mkataba mmoja.
Utolewaji wa Shahada na utiaji wa Saini wa hati za makubaliono 14 na mkataba mmoja, ni ishara ya kwamba, Uhusiano wa kihistoria baina ya Tanzania na India unazidi kuimarika.
Kuimairika kwa uhusiano huo, Mkoa wa Tabora unatarajia kufaidika na fursa za uwekezaji katika sekta ya Ulinzi, Nishati, Biashara, Madini na Usafirishaji.
Kwenye sekta ya Biashara Mkoa wa Tabora unategema zao la Tumbaku na Asali. Ambapo kwenye kilimo Mkoa umepata Bilioni 8.6 kwa ajili ya utolewaji wa Pembejeo za kilimo,hususani kilimo cha Tumbaku ili kuongeza kasi ya uzalishaji unaondana na mahitaji ya masoko ya kimataifa.
Mkoa wa Tabora umejiandaa na fursa zote zitakazopatikana baada ya ziara ya Mhe. Rais huko nchini India, kutokana na maboresho makubwa ya miundombinu ya barabara na reli ya kisasa (SGR) yanayoendea
Itakumbukwa kuwa, mpaka kufikia mwaka 2022 kupitia sekta ya biashara baina ya Tanzania na India kiwango cha biashara kilifika Dola za Kimarekani Bilioni 31. Na kuiweka India nafasi ya tatu kwa mataifa makubwa yanayoshirikiana na Tanzania kupitia sekta ya Biashara.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa