Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii wamekagua ukarabati wa Chuo cha Ufundi Stadi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu Luanzari, Tabora ambacho kilikuwa kimeacha kutumika kwa takribani miaka ishirini kwa sababu ya uchakavu wa miundombinu.
Kamati hiyo imefanya ukaguzi huo leo tarehe 12 Machi, 2024 ambapo wajumbe wallipongeza Serikali kwa hatua waliyochukua ya kukinusuru chuo hicho kwa kukarabati majengo hayo ambayo yalikuwa chakavu kwa muda mrefu.
Wakiwa chuoni hapo Wajumbe hao pia walijionea jinsi wanafunzi wenye Ulemavu wa aina mbalimbali wanavyofundishwa stadi mbalimbali.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako alieleza Kamati hiyo kuwamba Serikali imeweka mikakati ambayo itasaidia chuo hicho ambacho ni nyenzo muhimu kwa ajili ya kutolea mafunzo kwa Watu wenyewe Ulemavu kiendelee kutumika kama ilivyokusudiwa.
Kamati ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii ipo katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo na kesho inatarajiwa kuelekea Mkoani Mara kwa ajili ya kazi hiyo.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa