Mkuu wa mkoa wa Tabora Mh. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa ameambatana ma wajumbe wengine wakiongozwa na mwenyekiti wa CCM (M) Tabora Hassan Wakasuvi ambaye pia ni mjumbe wa (H) kuu taifa, katika ziara ya ukaguzi wa miradi ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2020. Katika ziara hiyo Dkt. Batilda alitoa pongezi na shukrani kwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye kwa miaka miwili amefanikiwa kutekeleza Ilani ya CCM kwa kasi kubwa sana hasa katika sekta ya Elimu, Miundombinu na Afya. Na ametoa pongezi kwa kamati yote ya siasa ya mkoa kwa kusimamia vema Ilani ya CCM ngazi ya mkoa.
Sambamba na hilo ametoa pongezi kwa watendaji wote wa serikali ngazi ya mkoa, wilaya,mbunge, kata na vijiji kwa kusimamia vema fedha za serikali. Na kama mkoa utaendelea kusimamia miradi yote ya maendeleo ili fedha zinazotolewa na Dkt. Samia Suluhu Hassan zionekakane thamani yake na kutoa huduma bora kwa wananchi. Ametoa wito kwa wananchi wa wilaya ya Igunga na Nzega kutunza na kulinda miundombinu ya barabara, afya na elimu ambayo serikali imewekeza fedha nyingi sana katika kuikamilisha. Ametoa wito kwa watendaji wa kijiji na kata kuwashirikisha wananchi wa eneo husika katika miradi ya maendeleo ili kuhakikisha wananchi hao wanahusika katika kulinda miradi hiyo.
Nao wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa kwa nyakati tofauti wamempongeza Mkuu wa mkoa wa Tabora kwa kusimamia vema miradi ya serikali ambayo ni sehemu ya Ilani ya CCM.Na kwamba kama viongozi wa Chama wanaridhishwa na utendaji wake na kuahidi kutoa ushirikiano kwa ofisi ya mkuu wa mkoa.
________________________
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa