• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KAMATI YATAKA SERIKALI ITOE FEDHA ZA KUMALIZIA MRADI MAKTABA KATIKA CHUO CHA ARDHI TABORA

Posted on: March 17th, 2020

WAJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi , Maliasi na Utalii wameitaka Serikali ipeleke fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi wa ujenzi wa Maktaba ya Chuo cha Ardhi Tabora.

Mradi huo ambao umekwama kumalizika kwa miaka saba unahitaji kiasi cha shilingi bilioni 1.1 ili kukamilika.

Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Flatei Massay alisema mradi umesimama siku nyingi ni vema Serikali ikatoa fedha za kumalizia ulipokwamia ili wanachuo waanze kunufaika.

Alisema fedha nyingi imeshatolewa na jengo bado halijakamilika jambo ambazo lizidi kusababishia wanachuo kukosa sehemu ya kujisomea.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mtama Nape Nnauye alisema ni vema Serikali ikatenga fedha katika bajeti ijayo ili ikiwezekana wakamilishe ujenze na ianze kutumika.

Alisema kila mwaka Bunge linapitisha fedha lakini hakuna kinachoendelea kwenye ujenzi wa mradi huo.

Mbunge wa Jimbo la Longido Dkt. Steven Kiruswa alikishauri Chuo kuangalia uwezekano wa kuandika andiko mradi kwa ajili ya kupata fedha zitakazowawezesha kukamilisha ujenzi huo.

Mbunge Jimbo la Chambani Yussuf Salim Hussein alihoji uwezo wa  Mkandarasi wa Jengo hili alipiga ripu kabla ya kueezeka ambapo fedha hizo angetumia kuezeka.

Alisema ni vema Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)  wanapopewa kazi ya kusimamia wakafanya vizuri badala kufanya kwa kiwango ambacho hakiridhishi .

Naye Mbunge wa Jimbo la Kaliua Magdalena Sakaya alisema ni vema Wizara ikaona umuhimu wa kukamlisha jengo hilo kwa ajili ya kuzalisha watalaamu ili kuziba mapengo kwenye Halmashauri mbalimbali hapa nchini.

Alisema wataalamu hao wanahitaji kwa ajili ya kusaidia kutatua matatizo na migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali.

Akijibu hoja za Wabunge hao Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula alisema kumekuwepo na miradi mingi ambayo inahitaji fedha ndio maana kumekuwepo uchelewaji baadhi yake kwa sababu ya ufinyu wa fedha.

Alisema miradi mingine iliyokwama inazaidi ya miaka 10 na yote inahitaji fedha ili iweze kukamilika na kuongeza kuwa Serikali ipo katika jitihada za kuikamilisha kwa kutegemea upatikanaji wa fedha.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa