Katibu Mkuu Ikulu, Ndugu. Maluli Mahendeka amewataka watumishi wa umma wa kanda ya magharibi inayohusisha mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma kufuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku. Ameyasema hayo leo februari 26, 2024, akifungua mafunzo kwa baadhi ya watumishi wa umma wa mikoa ya kanda ya magharibi kuhusu sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia utumishi wa umma yaliofanyika katika Ukumbi wa Isike Mwanakiyungi, Manispaa ya Tabora.
Katibu Mahendeka amesema kuwa “kuna ulazima wa kuzingatia sheria katika kutekeleza majukumu yenu ya kila siku kwa kuzingatia maadili, kujituma na kuwaheshimu na kuwathamini wateja wote mnaopaswa kuwahudumia”, alisema Katibu Mahendka
Ndugu. Mahendeka amesema kuwa, mafunzo haya yana manufaa mengi kwa mtumishi wa umma yakiwemo kuongeza uelewa katika utendaji wa kazi, kuongeza hali ya kujiamini katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku sambamba na kuondosha hali ya kufanya kazi kwa mazoea, na kutoa wito kwa watumishi hao kuyatumia mafunzo hayo katika kukamilisha malengo na faida za mafunzo hayo.
Aidha Katibu Mahendeka amewakumbusha watumishi wa umma kujua haki na wajibu ili kurahisisha upatikanaji wa ufumbuzi wa matatizo , malalamiko , kero na changamoto za wananchi ambao wanategemea huduma kutoka kwa watumishi hao.
Naye. Katibu Tawala Mkoa wa Tabora. Dkt. John Mboya ameishukuru serikali kwa kutoa mafunzo hayo kwa watumishi wa umma ambayo yamekuwa na tija katika kukuza weledi na uwajibikaji katika ofisi za umma.
Mafunzo kwa baadhi ya watumishi wa umma wa mikoa ya kanda ya magharibi kuhusu sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia utumishi wa umma yanatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku tano.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa