Katika Kuhakikisha Huduma za Afya zinawafikia Wananchi kwa urahisi Mkimbiza Mwenge Kitaifa 2023 Ndugu,Adallah Shaib Kaim leo Septemba 16, 2023 amezindua mradi wa Ujenzi wa Zahanati uliopo Kijiji cha Wachawaseme, Wilayani Kaliua, ujenzi huu umegharimu kiasi cha shilingi milioni 190, ambapo kiasi cha shilingi milioni 179.1 zilitoka Serikali kuu na Shilingi Milioni 11.1, ambapo jumla ya wananchi elfu 22 kutoka kijiji cha Wacha Waseme na elfu 7 kutoka kijiji cha Kazanaupate. Mradi huu umekamilika kwa asimia mia na tayari umeanza kutumika.
Kwa niaba ya Wananchi, Mbunge wa Jimbo la Kaliua Mhe. Aloyce Kwezi ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kutoa kwa ajili ya kuhimarisha huduma za afya. Na kwamba hapo awali wananchi walikuwa wakihangaika sana kupata huduma hizo, wakilazimika kutembea zaidi ya kilomita 10 kufata huduma za afya.
Akisoma taarifa ya mradi, Dkt. Amin Vasomana ameeleza kuwa, mpaka sasa tayari wakina Mama Wajawazito nane (8) wamejifungua, wagonjwa 123 wamepata huduma ya Baba Mama na Mtoto na wengine 137 wamepata huduma ya Wagonjwa wa nje (OPD).
Mradi huu wa Ujenzi wa Shule ya Msingi Dkt. Samia ni miongoni mwa miradi sita (6) ambayo imepitiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua. Ambapo Mapema leo Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Mhe. Dkt. Chuachua aliupokea kutoka Wilaya ya Tabora
Mwenge wa Uhuru uliwasili Mkoani Tabora Septemba 14, 2023 na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Kiloli, Wilayani Sikonge. ambapo utahitimisha mbio zake ukiwa umezindua jumla ya miradi 50 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 22.2 na kukabidhiwa Mkoa wa Singida Septemba, 21, 2023.
Kauli Mbiu ni "Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya maji kwa ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa