Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Simon Chacha ameyafungua rasmi Maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani katika viwanja vya Chipukizi, Manispaa ya Tabora leo Oktoba, 11, 2023.
Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Simon Chacha akisalimiana na baadhi ya viongozi kutoka taasisi mbalimbali zinazojihusisha na masuala ya kilimo zikiwemo TFRA na zinginezo zilizoshiriki kwenye maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani.
Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Simon Chacha akipata maelezo ya kina kutoka kwa mmoja wa watendaji kutoka Mamlaka ya Uthibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA). TFRA kama mdau mkubwa wa masuala ya Mbolea wana wajibu wa kuhakikisha mbolea zinawafikia wakulima kwa wakati na kwa uhakika, kwa mujibu wa taratibu, Sheria na miongozo iliyowekwa.
Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Simon Chacha akiwa kwenye banda la Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC) akipata maelezo kwa kina kutoka kwa mmoja wa watendaji wa (TCDC). TCDC ina wajibu wa kusimamia na kuhakikisha vyama vya msingi kupitia ushirika, mbolea inafika kwa wakati na ya kutosha. Sambmba na kusimamia na kudhibiti vyama vya ushirika nchini.
Baadhi ya wananchi kutoka Mkoa wa Tabora na Mikoa ya Jirani wakitembelea na kupata elimu, sambamba na kujionea shughuli mbalimbali katika baadhi ya mabanda yaliopo kwenye viwanja vya Chipukizi, kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani.
Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Simon Chacha akihutubia mamia ya wananchi waliopata kuhudhuria ufunguzi wa maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani kwenye viwanja vya Chipukizi vilivyopo Manispaa ya Tabora.
Katika hotubu yake Mhe. Simon Chacha alijikita kwenye kuelezea mafanikio makubwa yaliofanywa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kuhakikisha wakulima wanapata Mbolea ili kuongeza uzalishaji.
Maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani yameziduliwa leo Oktoba 11, 2023 na kufikia kilele chake mnamo Oktoba 13, 2023 ambapo inatarajiwa Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (Mb) kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha maadhimisho hayo.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa