Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amewaongoza mamia ya wanawake mkoani humo kusheherekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa ngazi ya mkoa yamefanyika katika viwanja vya Barafu, wilayani Igunga leo Machi 8, 2024
Akitoa hotuba yake, Mhe. Mkuu wa mkoa amewashukuru wanawake wote waliojitokeza kushiriki kwenye maadhimisho ambayo yamekuwa na mafanikio makubwa kwa wakazi wa mkoa wa Tabora na kutoa wito kwa wanawake hao kuendelea kuwa na umoja na mshikamano kuendeleza maadhimisho yanayofuata.
Mhe. Batilda Burian ametoa wito kwa wanawake kuwapeleka Watoto wenye umri chini ya miaka mitano (5) kwa ajili ya kupata chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kukabiliana na magonjwa yanayowakabili Watoto wenye umri huo ukiwemo ugonjwa wa surau.
Aidha Mhe. Mkuu wa Mkoa amemshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuwaunga mkono wanawake mkoani Tabora kwa kutoa vipaumbele vingi vyenye malengo ya kumuendeleza mwanamke.
Kauli mbiu inasema “Wekeza kwa Wanawake kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii”
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa