Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Zakaria Mwansasu akitoa salamu za Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, kwenye maadhimisho ya Kilele cha Sikukuu ya wakulima NANE NANE ambayo kwa kanda ya magharibi yamefanyikia hapa Mkoani Tabora.
Maadhimisho ya Sherehe za Wakulima (Nane Nane) hufanyika kuanzia tarehe 1 hadi 8 mwezi Agosti kila mwaka. Kitaifa maadhimisho haya yanafanyika katika viwanja vya John Mwakangale Manispaa ya Mbeya, ambapo leo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo kitaifa.
Kaulimbiu ya Nane nane mwaka 2023
“VIJANA NA WANAWAKE NI MSINGI IMARA WA MIFUMO ENDELEVU YA CHAKULA”.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa