BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Urambo limempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 2 za ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikwemo ya elimu na afya
Azimio hilo limesomwa jana na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Adam Malunkwi kwa niaba ya Madiwani wenzake wakati wa Kikao cha Baraza lao.
Alisema wao kama wawakilishi wa wananchi kutoka Kata mbalimbali wameguswa na kuvutiwa na mambo makubwa aliyowafanyia wakazi wa Urambo wa kuwapunguzia mzigo wa ujenzi wa miundombinu.
Malunkwi alisema kati ya fedha hizo ambazo ni shilingi bilioni 1.1 zitawasaidia kujenga vyumba vya madarasa 58 ya Sekondari na zaidi shilingi milioni 400 zitawasaidia kujenga vyumba 22 vya Shule Shikizi katika Kata mbalimbali za Wilaya hiyo.
Aliongeza kuwa shilingi milioni 300 zitajenga jengo la wagonjwa wa dharura katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo na kiasi cha shilingi milioni 160 zitajenga mabweni kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu.
Malunkwi alisema Rais Samia amewasaidia kuondokana na zoezi la kukimbizana kila ilipokuwa ikifika mwezi Desmba wa kutafuta michango kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya wananfunzi wanaoanza Kidato cha Kwanza.
Mwenyekiti huyo wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo aliwataka Madiwani wote kufuatilia kwa karibu ujenzi wa miundombinu itakayojengwa katika maeneo yao ili ilinganie na ubora ambao Rais Samia anatarajia.
Aliwataka wasimuone aibu ya kumchukulia hatua msimamizi ambaye watabaini kutekeza kazi zake chini ya kiwango kinachotakiwa
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa