Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Peter Bura amewahakikisha wajasiriamali mkoani Tabora kufaidika na mikopo inayotolewa na Benki ya CRDB kupitia programu ya iMBEJU. Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa ajili ya kuwaendeleza wanawake na vijana katika uvumbuzi yaliofanyika katika Ukumbi wa Utumishi wa Umma, Manispaa ya Tabora.
Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Bura ametoa wito kwa Benki ya CRDB kubuni namna mbalimbali za kutoa elimu kwa vijana na wanawake kuhusiana na matumizi ya huduma za kibenki ili mikopo wanayopata iwafaidishe katika shughuri zao za uzalishaji mali.
“Wapeni wateja wenu na wananchi wote kwa ujumla elimu ya umuhimu wa kuweka akiba, kukopa na kurejesha na kufanya malipo kupitia benki” alisema Mhe. Bura.
Aidha, Mhe. Bura amewataka vijana na wanawake wote kulipa madeni yako kwa wakati mara baada ya kupata mikopo ambayo wanaitumika kama mitaji katika kukuza mitaji yao ya biashara.
“Kwa wale ambao wana mpango wa kukopa, iwe mikopo binafsi au ya biashara, niwaombe kwa mara nyingine kutambua kuwa kurejesha kwao mikopo ndio kunaleta uendelevu wa Benki yetu hii”
Kwa upande wa mwakilishi wa Meneja Kanda ya Magharibi Ndugu. Asleim Mwenda amesema kuwa kwa mwaka huu Benki ya CRDB kupitia program ya iMBEJU, imetenga fedha za kutosha kwa ajili ya mikopo kwa vijana na wanawake katika kuwajengea uwezo katika shughuri zao za ujasiriamali na kutoa wito kwa vijana na wanawake kuchangamkia fursa hiyo.
Naye, Meneja wa CRDB tawi la Tabora Bw. Evodi Kereti amemuhakikisha Mkuu wa Wilaya ya Tabora kuwa, Benki ya CRDB imejipanga kutoa elimu kwa vijana na wanawake ili kuhakikisha mikopo inayotolewa kupitia program ya iMBEJU inakuwa na tija kwao.
Ikumbukwe kuwa, Programu ya iMBEJU inalenga kuimarisha biashara za ubunifu nchini Tanzania kwa kusaidia uvumbuzi ambao unachangia katika utengenezaji wa ajira kupitia kampuni za kuanzisha biashara. Wito huu unalenga kusaidia wanawake na vijana wabunifu kukua na kuweza kuuza bidhaa zao na huduma.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa